Friday, April 30, 2021

WAZIRI MHAGAMA ATEMBELEA NA KUKAGUA MAENDELEO YA MRADI WA NSSF JIJINI MWANZA


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama (kulia) akikagua maendeleo ya ujenzi wa Hoteli ya Nyota Tano “Mwanza Tourist Hotel” iliyopo eneo la Capripont Jijini Mwanza Aprili 30, 2021. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Tixon Nzunda, Katikati ni Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa NSSF, Bw. Masha Mshomba.

Mhandisi wa Mradi NSSF, Bw. Suleiman Salmin (kushoto) akifafanua jambo kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama alipotembelea eneo la mradi kwa lengo la kukagua maendeleo ya ujenzi wa Hoteli ya Nyota Tano “Mwanza Tourist Hotel” iliyopo eneo la Capripont Jijini Mwanza.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akisisitiza jambo kuhusu uendelezwaji wa mradi huo wakati wa kikao kazi cha kupokea taarifa ya utekelezaji wa mradi unaosimamiwa na NSSF wa Ujenzi wa Hoteli ya Nyota Tano iliyopo Jijini Mwanza.

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Bw. Tixon Nzunda (kulia) akieleza jambo wakati wa kikao hicho.

Sehemu ya Watendaji kutoka NSSF na Ofisi ya Waziri Mkuu wakifuatilia maelekezo ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama (hayupo pichani) alipotembelea mradi huo wa ujenzi wa Hoteli ya Nyota Tano “Mwanza Tourist Hotel” iliyopo eneo la Capripont Jijini Mwanza.

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Bw. Tixon Nzunda (kulia) na Naibu wake Prof. Jamal Katundu (kushoto) wasikiliza maelekezo ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama (hayupo pichani) wakati wa kikao kazi hicho.

Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa NSSF Bw. Masha Mshomba akifafanua jambo kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama alipotembea na kukagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa Hoteli ya Nyota Tano “Mwanza Tourist Hotel” iliyopo eneo la Capripont Jijini Mwanza.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akitoa maelekezo kwa Katibu Mkuu wa ofisi hiyo Bw. Tixon Nzunda (kushoto), Naibu Katibu wake Prof. Jamal Katundu pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa NSSF Bw. Masha Mshomba wakati wa majumuisho ya ziara yake.

Muonekano wa jengo la Hoteli ya Nyota Tano “Mwanza Tourist Hotel” iliyopo eneo la Capripont Jijini Mwanza.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akiwa kwenye picha ya pamoja na Watendaji kutoka Ofisi yake na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii NSSF alipotembelea na kukagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa Hoteli ya Nyota Tano “Mwanza Tourist Hotel” iliyopo eneo la Capripont Jijini Mwanza.

PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU

(SERA, BUNGE, URATIBU, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU)

 

No comments :

Post a Comment