……………………………………………………………………..
NA NAMNYAK KIVUYO, ARUSHA
Walimu wakuu wa shule
za msingi wametakiwa kutumia mafunzo waliyoyapata kurekebisha matatizo
yaliyopo katika shule wanazoziongoza na sio kusubiri watu wa nje kwenda
kufanya kazi hiyo.
Rai hiyo imetolewa na mtendaji mkuu wa wakala wa
maendeleo ya uongozi wa elimu(ADEM) iliyo chini ya wizara ya elimu Dkt
Siston Masanja wakati akifunga mafunzo ya udhibiti ubora yaliyotolewa
kwa walimu zaidi ya 300 kutoka halmashauri 7 za mkoa wa Manyara.
Dkt Masanja alisema ni mategemeo kuwa walimu
waliopata mafunzo hayo kwa awamu ya Kwanza wataenda kutumia maarifa hayo
katika kudhibiti ubora wa taaluma na maendeleo ya shule kwa ujumla.
Alieleza hawapaswi kwenda kukaa ofisini tuu bali
wakafuatilie kila kinachoendelea katika shule zao ikiwemo ufundoshaji
ambapo kwa kufanya hivyo ndani ya miezi sita kutakuwa na mabadiliko
makubwa.
“Kahakikisheni mnashughulikia yale yote mnayoona
mnastahili kwa kufanya maamuzi yatayoleta matokeo chanya na sio mkakae
kusubiri watu kutoka nje waje kutatua changamoto wakati nyie mpo na
uwezo wa kutatua mnao,” Alisema Dkt Masanja.
Alifafanua kuwa kudhibiti ubora ni pamoja na
kurekebisha mambo ndani ya shule zao na kuangalia namna wanavyowaongoza
walimu wao kwa kufiatilia kama wanaadaa mpango kazi au wanatumia ya
miaka iliyopita na kama hawaandai waangalie ni namba gani wanaweza
kuwasaidia ili wanafunzi waweze kupata elimu sahihi na kuweza kuinua
kiwango cha elimu.
Mratibu wa mafunzo hayo Malimi Sai alisema
kuwa walimu hao wamepata mafunzo juu ya udhibiti ubora wa shule,
ufunfishaji, mtaala, ufuatiliaji , tasmini na mengineyo ambapo wanaamini
kuwa mafunzo hayo yamewapa umahiri mkubwa wa kwenda kisimamia shule
zao.
Kwa upande wake mkuu wa chuo Patandi elimu
maalum Lucian Segesela alieleza kuwa wakala wa maendeleo ya uongozi wa
elimu (ADEM) ni mkombozi sahihi katika masuala yanahusu udhibiti wa
ubora wa elimu kwani hata katika ngazi ya chuo walishapata mafunzo yenye
weledi mkubwa kwaajili ya kuimarisha usimamizi.
Nae mmoja wa walimu hao Nyanda Steven kutoka
halmashauri ya mbulu alisema kuwa mafunzo hayo yameweza kuwanufaisha
kwani wamegundua kuwa wao ni wadhibiti namba moja katika maeneo ya shule
ambapo wamejua kuwa wanafunzi, walimu,wazazi na jamii kwa pamoja
wanaweza kutoa tathimini zinazoweza kuboresha shule.
“kwa kweli mafunzo haya ni mazuri yatatusaidia
kuboresha shule kwanzia ngazi kata hadi taifa na hata kwa wale wenzetu
ambao hawakupata haya mafunzo tutaenda kuwafundisha na wao ili kiwango
cha elimu kiweze kuinuka,” alisema mwaalimu Nyanda.
Hata hivyo mafunzo hayo yanefanyika katika Chou cha ualimu Patandi Mkoani Arusha kwa mada wa siku tatu.
No comments :
Post a Comment