Friday, February 12, 2021

TAARIFA: KUKAMATWA KWA RAIA 10 WA BURUNDI KWA KOSA LA KUINGIA NCHINI BILA KIBALI

Mnamo tarehe 15.12.2020 JESHI la Polisi Mkoa wa Mbeya kwa kushirikiana na Idara ya Uhamiaji lilimefanikiwa kuwakamata wahamiaji haramu 57 wote raia wa Ethiopia kwa kosa la kuingia nchini bila kibali.

JESHI la Polisi Mkoa wa Mbeya limefanikiwa kuwakamata raia wa Burundi 05 wakiwa na watoto wao 05 kwa kosa la kuingia nchini bila kufuata taratibu za nchi.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamanda wa polisi Mkoa wa Mbeya SACP Ulrich O. Matei imeeleza  kwamba tarehe 10.02.2021 majira ya saa 12:30 mchana huko kijiji na kata ya Changalawe, Tarafa Kiwanja, wilaya ya Chunya, Mkoa wa Mbeya . Askari Polisi wakiwa doria walisimamisha  Basi la abiria yenye namba T.353 ANS inayomilikiwa na Kampuni AN ikitokea Mkoa Tabora kwenda Mbeya.

Askari walianza kufanya ukaguzi kwenye basi hilo na ndipo walimkamata NDAYIPEUKAMIYE  SADOCK [37] Raia na Mkazi wa nchini Burundi  akiwa na wenzake 04 pamoja na watoto wao 05 kwa kosa la kuingia nchini bila kibali. Taratibu za kuwafikisha mahakamani zinaendelea.

 

 

No comments :

Post a Comment