…………………………………………………………………………..
NA NAMNYAK KIVUYO, ARUSHA.
Kampuni
inayojishughulisha na upimaji wa udongo kwa wakulima wakubwa,wakati na
wadogo(LSSL)imeiomba serikali kupitia maafisa ugani kutoa elimu kwa
wakulima juu ya umuhimu wa afya ya udongo.
Akiongea na waandishi
was habari mkurugenzi wa kampuni hiyo Dkt Edmond Matafu alisema kuwa
bado wakulima wengi hawana ulewa juu ya afya ya udongo ambayo ndio
msingi mkubwa wa kilimo.
Alisema elimu bado
haijawafikia wakulima walio wengi hali inayopelekea kutokuona umuhimu wa
kupima udongo na kuendelea kulima kilimo cha mazoea kisichokiwa na
tija.
Dkt Matafu alieleza
kuwa Kuna faida kubwa za kupima udongo moja wapo ikiwa ni kujua aina ya
mazao yanayofaa katika shamba la mkulima, kujua virutubishi vilivyopo
katika udongo na ni kwa kiasi gani, pamoja na mkulima kununua mbole
kulingana na upungufu wa virutubishi vinavyohitajika kwenye udongo.
“Hii itasaidia
kupunguza gharama kwani wakulima wamekuwa wakitumia mbolea hata kwa
mashamba ambayo yana virutubisho vya kutosha na wakati mwingine kutumia
mbolea isiyofaa kwa eneo husika jambo linaloongeza gharama na kuleta
hasara kwa kutokupata mazao ya mimea aliyootesha,”Alisema Dr Matafu.
Alifafanua kuwa
faida nyingine ni kusaidia kutunza mazingira kwasababu baadhi ya
virutubishi vikizidi kwenye udongo huweza kuharibu mazingira na kufanya
mimea ya aina yoyote isiweze kuota ambapo mkulima atakapo pima udongo
katika shamba lake atajua mahitaji ya mbolea au virutubishi
vinavyohitajika na kujua jinsi ya kuboresha udongo huo.
Alieleza kuwa lengo
la kuhamasisha upimaji wa udongo ni ili kuwasaidia wakulima wote nchini
kujua afya ya udongo hasa tindikali (PH), kujua virutubishi vilivupo
katika udongo kabla ya kulima zao lolote na kuwezesha kujua kias i cha
mbolea inayojitajika katika mmea.
“Kwa kupima udongo
mkulima atajua virutubishi vilivyoko kwenye udongo Kama vile Organic,
Carbon, Nitrogen, Sodium, potassium pamoja na virutubisho vidogo vidogo
ambavyo ni muhimu kwa ukuaji na uzalishaji wa mmea Kama vile boron,
zinc, copper, Cobalt, silicon na kuendelea,” Alieleza.
Alifafanua kuwa ni
muhimu kwa wakulima kabla ya kulima au kuotesha kujua kujua afya ya
udongo wa shamba lake ili kuweza kufanya kilimo chenye tija ambapo
anatakiwa kuchukua sampuli ya udongo kwa njia ya kupshanisha (zigzag)na
kupeleka katika maabara ili kujua aina ya mbolea na mazao yanayokubali
katika eneo hilo.
“Majibu mazuri ya
udongo yanatokana na umakini wa uchukuaji wa sampuli katika shamba
ambapo anayechukua udongo anatakiwa kuchima vishimo zaidi ya 15 vyenye
kina Kati ya sentimita 15 hadi 20 na kukusanya sapuli hizo toka maeneo
mbalimbali ya shama analotarajia kulima,”alifafanua.
Aliendelea kusema
kuwa baada ya kukamilika kwa zoezi la ukusanyaji wa sampuli, udongo huo
utapelekwa katika maabara ambapo majibu yake yatatoka baada ya siku
kaadhaa lakini pia kina kifaa cha kupima udongo papo kwa hapo.
“LSSL tuna aina mbili
za teknolojia za kupima udongo moja ya papo kwa hapo na nyingine ni ya
maabara ambapo hii ndio inayotoa majibu mengi zaidi ikiwa ambayo Ni
pamoja na aina ya mazao yanayofaa katika shamba lakini Kuna maeneo
mengine pia majibu yanatoka kuwa hapafai kulima zao lolote na hapa
panahitajika jitihada za kurutubisha udongo,” Alisema
“Kuna madhara
unapoweka mbolea mahalo pasipo hitaji mojawapo ikiwa ni kuharibu udongo
na kupunguza uzalishaji wa mazao na sisi LSSL tunapima udongo ili
kusaidia wakulima kuongeza tija ya mazao wanayozalisha,”alibainisha.
Kwa upande wake Alen
Andrew meneja masoko wa kampuni hiyo alisema kuwa kampuni hiyo inafanya
kazi nchi mzima ambapo asilimia kubwa ya wakulima waliojitokeza kupima
udongo wao ni kutoka nyanda za juu kusini na katika meneo mengine mwamko
bado ni mdogo.
“Hii ni huduma mpya
wengi bado hawana uelewa ww umuhimu wa kupima udongo lakini nisisitize
kuwa kutumia mbegu Bora na mbolea bila kufahamu afya ya udongo hakiwezi
kuleta tija,”Alieleza Alen.
Alieleza ikumbukwe
kuwa udongo ndio msingi wa kilimo hivyo wakulima wawekeze kwenye afya ya
udongo ili waweze kulima kilimo Bora chenye manufaa kwao na kwa taifa
zima.
Alisema teknolojia
waliyonayo inauwezo wa kupima udongo kwa haraka zaidi bila kuhitaji
kenikali ambapo kwa siku wanaweza kupima sampuli zaidi ya 50.
No comments :
Post a Comment