Monday, February 1, 2021

HATIMAYE TARURA YACHONGA BARABARA YA MAGENGENI KIJICHI BAADA KUMALIZIKA KWA MGOGORO

Hatimaye mtambo wa kuchonga Barabara umewasili Kata ya Kijichi mtaa wa Butiama kitongoji Magengeni na kuanzia Kazi ya kuchonga Barabara hiyo iliyokaa muda mrefu bila matengenezo kutokana mgogoro uliodumu kwa miaka 15 ambapo mmoja wa wananchi aitwaye Cripin Bulamu aliziba Barabara hiyo na kuibua mgogoro na wananchi wenzake pamoja na kuhangaika kwa muda mrefu hatimaye kwa msaada wa Mkuu wa wilaya ya Temeke Bw.Godwin Gondwe aligiza afisa Ardhi wilaya ya Temeke kufika eneo la tukio kuona Hali ilivyo ndipo serikali ikaagiza wananchi kuifungua Barabara hiyo ambapo sasa wakala wa Barabara Vijijini TARURA wameanza kuichonga leo Jumatatu Februari 1,2021.

No comments :

Post a Comment