Mwanzilishi
wa Taasisi ya Keep Life, Sophia Mbeyela akiongoza katika maandamano
ikiwa ni moja ya kusheherekea siku ya walemavu duniani ambayo hufanyika
kila mwaka ifikapo Desemba 3. Maandamano hayo yamianzia Kituo cha polisi
Oysterbay jijini Dar es Salaam hadi Kituo cha Donibosco.
Mwanzilishi wa Taasisi ya Keep Life, Sophia Mbeyela
Mwanzilishi
wa Taasisi ya Keep Life, Sophia Mbeyela akizungumza na waandishi wa
habari jijini Dar es Salaam leo mara baada ya maandamano kwaajili ya
kuadhimisha siku ya watu wenye ulemavu duniani.
Na Mwandishi wetu Globu ya Jamii
IKIWA
ni miaka 28 sasa tangu kuanzishwa kwa maadhimisho ya siku ya watu wenye
ulemavu duniani ambayo hufanyika kila mwaka ifikapo Desemba 3, 2020
watu wenye ulemavu nchini Tanzania bado walia na miundombinu rafiki ya
vyoo kwa watu wenye ulemavu.
Ili
kuhakikisha watu wenye walemavu wanapata haki sawa kama watu,
Mwanzilishi wa Taasisi ya Keep Life, Sophia Mbeyela amehamasisha jamii
kujenga Vyoo rafiki kwa watu wenye ulemavu nchini hasa mashuleni.
Akizungumza
na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo Desemba 5, 2020,
amesema kuwa katika kudhimisha siku ya watu wenye ulemavu dunia ambayo
hufanyika kila mwaka Desemba 3, kwa mwaka huu wamejikita katika
kuhamasisha ujenzi wa vyoo rafiki hasa mashuleni kwaajili ya wanafunzi
walemavu wanaopata huduma ya elimu hapa nchini.
"Kwa
sababu sasa hivi jamii kubwa imeelimika kupeleka watoto wenye ulemavu
mashule kwahiyo tunaomba serikali na jamii nzima tuungane pamoja katika
kuhakikisha upatikanaji wa vyoo rafiki mashuleni vinapatikana." Amesema
Sophia.
Hata hivyo Sophia amewahamasisha walemavu wajikite katika kupambana kukuza uchumi wao binafsi na uchumi wa Taifa kwa Ujumla.
Akizungumzia
hali ya sasa na ya kipindi cha nyuma cha upatikanaji wa haki kwa watu
wenye ulemavu Sophia amesema kuwa angalau haki zimeanza kutekelezwa japo
kiwa sio kwa asilimia 100.
"Kwahiyo
sisi kama wadau wa watu wenye ulemavu tunaihamasisha jamii, serikali na
wadau wote tuendelee kupambana ili kuhakikisha haki za watu wenye
ulemavu zote zinatekelezwa kama haki za watu wengine."
Hata
hivyo Sophia ametoa wito kwa jamii kiwatambua watu wenye ulemavu popote
pale walipo na kuhakikisha wanapata fursa sawa hasa Elimu ya Afya ya
Uzazi, elimu ya Masuala ya unyanyasaji wa kijinsia kwa watu wenye
ulemavu.
Pia kuhakikisha jamii inawajumuisha walemavu kwa vitendo kupata elimu na stahiki zote zinazojitokeza katika jamii.
Kwa
upande wake, Mzazi mwenye mtoto mwenye ulemavu, Agnes Mbeyela ameomba
viongozi wa serikali kuanzia serikali ya mtaa mpaka serikali kuu
kuwaingiza wazazi wa watoto wenye ulemavu katika Mfuko wa kusaidia kaya
masikini (TASAF)..
"Familia za watoto wenye
ulemavu wanahangaika sana hadi imefikia kipindi wanawaweka watoto
barabarani ili wapate chochote, kwahiyo wawaingize kwenye kaya masikini
nawaomba serikali." Amesema Agnes
No comments :
Post a Comment