Tuesday, December 8, 2020

DKT.PIUS MSEKWA ATUNUKIWA SHAHADA YA HESHIMA YA UDAKTARI KATIKA MAHAFALI YA 50 UDSM

Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiteta jambo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) katika mahafali ya 50 ya chuo hicho yaliyofanyika jijini Dar es Salaam

Baadhi ya Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa Nchini wakifuatilia sherehe za mahafali ya 50 ya chuo hicho yaliyofanyika jijini Dar es Salaam

Baadhi ya wahitimu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wakiwa ukumbini tayari kwa ajili ya kutunukiwa shahada katika mahafali ya 50 ya chuo hicho yaliyofanyika jijini Dar es Salaam

Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimtunuku shahada ya heshima Naibu Waziri Mkuu Wa Jamhuri ya Namibia ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Namibia, Mhe. Netumbo Ndaitwah

Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi moja kati ya zawadi Naibu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Namibia ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Namibia, Mhe. Netumbo Ndaitwah

Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimtunuku shahada ya heshima Dkt. Pius Msekwa katika mahafali ya 50 ya chuo hicho yaliyofanyika jijini Dar es Salaam Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi moja kati ya zawadi SPIKA wa Bunge Mstaafu, Dkt. Pius Msekwa katika mahafali ya 50 ya chuo hicho yaliyofanyika jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiwasilisha salamu za Serikali kwenye mahafali ya 50 ya chuo hicho yaliyofanyika jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akimkabidhi zawadi ya vitabu Naibu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Namibia ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Namibia, Mhe. Netumbo Ndaitwah.

Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akipata picha ya pamoja na Spika wa Bunge Mstaafu, Dkt. Pius Msekwa,Naibu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Namibia ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Namibia, Mhe. Netumbo Ndaitwah,Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Profesa Palamagamba Kabudi,Makamu Mkuu wa Chuo hicho Profesa William Anangisye pamoja na viongozi wengine katika mahafali ya 50 ya chuo hicho yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.

*************************************

Spika wa Bunge Mstaafu, Dkt. Pius Msekwa, amesema shabaha ya elimu ya juu katika maisha ya sasa ni kumkomboa binadamu kifikra na kumpa uwezo wa kujisimamia, sio kuajiriwa na Serikali kama inavyodhaniwa na wengi. 
Amesema kulingana na tafsiri hiyo ni muhimu wahitimu wakaondoa fikra na mitazamo ya kuajiriwa na serikali na badala yake wajiandae kuitumikia nchi kwa namna yoyote halali watakayobuni wenyewe. 
Dkt. Msekwa, aliyasema hayo baada ya kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Udaktari wa Sheria, wakati wa hafla ya Mahafali ya 50 duru ya tatu ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam tawi la Mwalimu Nyerere. 
Alisema awali tafsiri ya elimu ilikuwa ni kuajiriwa na serikali na hata mfumo wa mafunzo ulifanyika kufanikisha hilo.
Dkt. Msekwa, alisema kwa wakati huo hata majukumu ya Chuo Kikuu yalikuwa ni kuandaa wataalamu kwa ajili ya utumishi wa umma na idara nyingine za serikali.
Aliongeza kuwa hata idadi ya wanafunzi waliodahiliwa ilifanyika kulingana na mahitaji ya watumishi tu.
“Wakati huo kusoma chuo kikuu ilikuwa haki ya wateule wachache kwa ajili ya kuitumikia serikali na idara nyingine za umma,” alisema. 
Kulingana na Dkt. Msekwa, wahitimu wakati huo walikuwa na uhakika wa ajira.
Alisema hayo yalibadilika baada ya kufanyika kwa mabadiliko ya sera kutoka elimu kuwa haki ya wateule wachache na kuwa haki ya watu wote. 
“Hii ilibadili majukumu ya vyuo vyetu, kutoka kutoa elimu kwa waajiriwa hadi kutoa elimu ya kuwakomboa fikra na tafsiri hiyo ndiyo iliyotumika wakati wa Azimio la Arusha na ikazaa neno ‘Elimu ya Kujitegemea’, ” alisema.
Alitaka wahitimu kujiandaa kifikra katika uhalisia wa tafsiri ya elimu kwa sasa na waondokane na mitazamo ya kuajiriwa. 
Kwa upande wake Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Profesa Palamagamba Kabudi, alisema Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kinatarajiwa kupokea Dola milioni moja kila mwaka kwa miaka 10 kutoka Kampuni ya Barrick Ltd, kwa lengo la kuendeleza kitivo cha Madini kilichoanzishwa chuoni hapo. 
Alisema hatua hiyo ni kulingana na baadhi ya vipengele vya mkataba Kati ya serikali na Kampuni hiyo ambapo UDSM itakuwa ikipewa Dola milioni moja kila mwaka kwa kipindi cha miaka 10. 
“Hii tumelenga ikatumike kuboresha taaluma ya madini inayotolewa katika chuo kikuu cha Dar es Salaam, ukizingatia hii ni miongoni mwa taaluma mpya zilizoanzishwa chuoni hapa,” alisema. 
Nae Makamu Mkuu wa Chuo hicho Profesa William Anangisye, alisema hiyo ni mahafali ya 50 kufanyika tangu kuanzishwa kwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. 
Alisema chuo hicho kitaendelea kushirikiana na TAASISI nyingine za kimataifa katika kuboresha utoaji wa taaluma.
Prof. Anangisye Alitaka miongoni mwa mafanikio ealiyopitia chuoni hapo ni pamoja na kuongezeka kwa bajeti ya utafiti kutoka sh. bilioni 1.4 mwaka 2019 hadi sh. bilioni 1.9 mwaka huu. 
Pia alisema katika mahafali hiyo wameamua kuwatunuku shahada za heshima za Udaktari Pius Msekwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Namibia Netumbo Ndaitwa, ikiwa no ishara ya kutambua mchango wao katika mapambano ya mambo mbalimbali ikiwemo Diplomasia, Uhuru na utumishi uliotukuka.

 

No comments :

Post a Comment