Wakili Sylvester Temu akiongea na wanahabari hawapo pichani kwenye banda la Kampuni hiyo mapema leo kwenye kongamano la wanasheria TLS linalofanyika kwenye Hotel ya Lush Garden wilayani Arumeru picha zote na Ahmed Mahmoud Arusha
Bango linaloonyesha mfano wa kadi kwa ajili ya kupata huduma kwa njia ya mtandao wa tehama kama ilivyokutwa na kamera ya matukio kwenye banda ya kampuni hiyo mapema leo wilayani Arumeru.
Familia bora baada ya kuandika wosia kama inavyoonekana kwenye Bango la kampuni ya ABC ATTORNEY kwenye viwanja vya hotel ya Lush Garden wilayani Arumeru mapema leo picha zote na Ahmed Mahmoud Arusha
……………………………………………………………………………
Na Ahmed Mahmoud Arusha
Kampuni ya ABC
ATTORNEYS yenye makazi yake jijini Dar es Salaam imezindua huduma ya
tehama kwa kadi za kieletroniki kwa wateja wake itakayosaidia kupata
huduma bila kufika ofisini kwao.
Akiongea mapema leo
mwakilishi wa kampuni hiyo wakili Sylvester Temu kwenye maonyesho
yalioenda sambamba na kongamano la siku Tatu la chama cha wanasheria
Tanganyika TLS ameeleza
kuwa upo umuhimu na faida ya kuwa na kadi hizo.
Alisema kuwa kadi
hizo zine faida kwa kumsaidia mteja wao kujua mwenendo wa maendeleo ya
kazi aliyoipatia kampuni tena kwa muda wowote na mahali popote nchini.
Kwa mujibu wa wakili
Temu kadi hizo pia inasaidia mteja wetu kupata points na baadae
kufanikiwa kufanyiwa kazi bila malipo pindi atakapokuwa mteja kwa muda.
Faida nyingine ni mteja wetu kuweza kufanya mawasiliano na wanasheria wake bila kufika ofisini kwetu.
Akizungumzia suala la
kuandika wosia wakili Temu alisema kuwa utoaji wa mafunzo ya kuandika
wosia ili kuwa na furaha katika familia pia wosia unasaidia kulinda
familia yako na kulinda Mali yako.
Alisema bado kwenye
suala la kuandika wosia kumekuwa na changamoto kwa jamii kudhani kuwa
wakiandika basi ndio watakufa hilo halina ukweli wosia humsaidia mteja
kulinda mali zake na familia yake.
No comments :
Post a Comment