Afisa
Takukuru Kanda ya Ilala jijini Dar es Salaam, Bi. Marcela Sallu akitoa mada kwa
waajiriwa wapya katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kuhusu kanuni, sheria
taratibu za utumishi wa umma. Baadhi ya watumishi wa MNH walishiriki pia semina
hiyo.
Mmoja wa waajirwa wapya akisikiliza kanuni, sheria taratibu za utumishi wa umma.
Wafanyakazi wapya 68 wameajiriwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) katika ngazi mbalimbali sambamba na kupatiwa mafunzo ya maadili ya utumishi wa umma na kutoa huduma bora kwa wagonjwa.
Katika mafunzo hayo, wafanyakazi hao wametakiwa kuazingatia sheria, kanuni na taratibu za kazi na kutojihusisha na masuala ya rushwa ambayo inachelewesha na kuzuia utoaji bora wa huduma za afya.
Mkuu wa Idara ya Ajira na Mafunzo wa Muhimbili, Bw. Abdallah Kiwanga amesema hospitali imeajiri wataalamu wa macho, wataalamu wa tiba ya viungo, wahudumu wa afya, wauguzi, wauguzi wasaidizi, watunza kumbukumbu na wataalamu wa maabara.
No comments :
Post a Comment