Tuesday, November 10, 2020

Serikali kuwachukulia hatua kali wanaopandisha bei ya saruji



Serikali imesema itawachukulia hatua kali za kisheria, ikiwemo kuwanyang’anya leseni wale wote watakaobainika kuuza saruji kwa bei ya juu.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa mkoa wa Tanga Martine Shigella, mara baada ya kutembelea viwanda vya Saruji vilivyopo jijini Tanga na kukuta uzalishaji ukiendelea.

Amesema bei ya kiwandani ni kati ya shilingi elfu kumi na mia sita (10,600) kwa mkoa wa Tanga na nje ya mkoa ni shilingi elfu kumi na moja na mia sita (11,600) kwa mfuko moja.

Aidha amesema kutokana na kutokuwepo kwa ongezeko la bei kutoka viwandani ya bei ya saruji itabaki kama ilivyokua awali na si vinginevyo

 

No comments :

Post a Comment