Thursday, November 5, 2020

BARAZA LA MAWAZIRI KUKOMA SHUGHULI ZAKE LEO


Na Richard Mwaikenda, Dodoma

BARAZA la Mawaziri limekoma leo kuendelea na shughuli za

kikazi mara atakapoapishwa Rais Mteule, Dk. John Magufuli kwenye Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma .

Taarifa hiyo imetolewa na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dk. Hassan Abbas alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari jijini Dodoma jana, kuhusu kukamilika kwa maandalizi ya kuapishwa kwa Rais Mteule, Dk Magufuli.

Dk Abbas alisema kuwa kisheria ni kwamba  Baraza la Mawazili la 2015-2020 mwisho wake ni mara tu Rais Mteule atakapoapishwa kushika kipindi chake cha pili cha miaka mitano. Majukumu yote yatafanywa na makatibu wakuu wa wizara hadi atakapotangaza baraza jipya.

 

No comments :

Post a Comment