Thursday, October 1, 2020

UBALOZI WA TANZANIA - KOREA KUSINI WAANDAA SHINDANO LA 'SHOW ME TANZANIA PHOTO CONTEST EVENT' KUTANGAZA UTALII WA TANZANIA

.
Balozi wa Tanzania Korea Kusini, Mhe. Matilda Swilla Masuka, akimkabidhi zawadi ya kinyago huku akitoa maelezo mafupi ya maana ya kinyago hicho Bw. Donghee Choi, katika ofisi za Ubalozi wa Tanzania jijini Seoul.
Mhe. Balozi Matilda Swilla Masuka akimkabidhi zawadi ya Tingatinga mshindi wa kwanza wa shindano la “Show Me Tanzania” Bw. Donghee Choi, katika ofisi za Ubalozi wa Tanzania jijini Seoul.
Balozi wa Tanzania Korea Kusini, Mhe. Matilda Swilla Masuka na wafanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania, Seoul wakibalishana mawazo na Bw. Donghee Choi jinsi ya kuitangaza zaidi “Destination Tanzania”. Bw. Donghee Choi ni “Travel blogger” maarufu hapa Seoul na amekuwa akisafiri nchi mbalimbali duniani.
Balozi wa Tanzania Korea Kusini, Mhe. Matilda Swilla Masuka akikabidhi zawadi ya vikombe vyenye kutangaza utalii wa Tanzania na kahawa kutoka Tanzania kwa mshindi wa pili wa shindano la “Show Me Tanzania” bwana Suho Lee, katika ofisi za Ubalozi wa Tanzania jijini Seoul.
Balozi wa Tanzania Korea Kusini, Mhe. Matilda Swilla Masuka akikabidhi “Plaque of Appreciation” kwa mshindi wa kwanza wa shindano la “Show Me Tanzania” Bw. Donghee Choi, katika ofisi za Ubalozi wa Tanzania jijini Seoul
Mhe. Balozi Matilda Swilla Masuka akimkabidhi zawadi ya Tingatinga mshindi wa pili wa shindano la “Show Me Tanzania” Bw. Suho Lee, katika ofisi za Ubalozi wa Tanzania jijini Seoul.
Mshindi wa pili wa shindano la “Show Me Tanzania” bwana Suho Lee, akipiga picha ya vivutio mbalimbali vya utalii vilivyopo Tanzania kwa ajili ya kuzitumia katika mitandao yake ya kijamii. Bw. Suho Lee ni Mwandishi maarufu wa habari za kitalii hasa utalii wa nchi za kiafrika. 


====== ======== ======== ========

“SHOW ME TANZANIA PHOTO CONTEST EVENT”

Katika juhudi za kuwavutia watalii zaidi kutembelea Tanzania, Ubalozi wa Tanzania, Korea Kusini ulibuni Shindano la “Show Me Tanzania” ambapo Wakorea waliowahi kutembelea Tanzania walikuwa wanatuma picha walizopiga wakiwa katika vivutio vyetu mbalimbali kupitia Akaunti yetu ya Instagram- tanzaniaembassykorea

Shindano hilo lililokuwa la siku 10, kuanzia Agosti 31 hadi Septemba 10, lilikuwa la mafanikio makubwa kwa kuwavutia washiriki 154 ambao waliposti zaidi ya picha 1100 na kupata likes zaidi ya 37,000. Kwa maana nyingine katika muda wa siku hizo kumi Ubalozi uliweza kuongeza wafuasi wapya 300 katika mitandao yetu ya kijamii na kuwafikia zaidi ya watu 37,000 ambao waliziona picha hizo zenye kuonyesha uzuri wa vivutio vyetu vya utalii, ubora wa huduma za mahoteli, vyakula, na ukarimu wa Watanzania. 

Aidha, shindano hilo limewachagiza hata wale waliowahi kutembelea Tanzania kuweka nia ya kurejea tena nchini kwa kuona kwamba kumbe kuna sehemu nyingine nzuri pia ambazo hawakuweza kutembelea na hivyo kuwapa hamasa upya ya kutembelea tena Tanzania. 

Kwa upande mwingine picha zilizokuwa zikitumwa zimedhihirisha dhana ya 3600 kwani ziligusa maeneo mbalimbali yakiwemo Mlima Kilimanjaro, Beaches za Zanzibar, Dar es Salmaam, Bagamoyo, Safari za Mbugani, Spice Tour, Maeneo ya Kihistoria kama Kilwa, Stone Town nk. Kwa uhakika shindano lilifana sana na kujidhihirisha Destination Tanzania inajitosheleza. 

Kwa ujumla wake, shindano hilo limeongeza hamasa ya watalii kuja kutembelea Tanzania, limetuongezea wafuasi wetu katika mitandao ya kijamii, limefanya baadhi ya makampuni ya utalii kuanza kushirikiana nasi kama Ubalozi ambapo tumepata timu ya bloggers na influencers ambao tunaweza kuwatumia tunapotaka kuwafikia watu wengi zaidi kuhamasisha suala zima la Utalii. 

Kupitia Shindano hili Ubalozi umeendeleza juhudi za kuwavutia wageni hawa kuja kutembelea Tanzania. Juhudi zingine ni Pamoja na: Ufunguzi wa Blog ya Kikorea kupitia mtandao wa Naver, ambayo inawafikishia Habari kwa lugha ya Kikorea; na pia Media FAM Tour iliyofanyika mwishoni mwa mwaka jana ambapo kampuni 10 (Media, Bloggers and Influencers) walitembelea Tanzania na kujionea vivutio vya utalii na baada ya kurudi kuandika Makala kwa muda wa miezi sita. 

Makala hizo zimekuwa chachu na hamasa kubwa kwa umma wa Wakorea. Tunaamini, kwa kupata Safe Travels Stamp na uwepo wa Standard Operating Procedures (SOPs), hali ikitengamaa kwenye hizi nchi za wenzetu, tutaanza kupokea wageni wengi zaidi katika eneo hili la utalii.

 

No comments :

Post a Comment