Jengo ambalo benki ya Mucoba Plc ipo na kufanyika uzinduzi wake siku ya kesho iringa mjini.
……………………………………………………………………….
NA DENIS MLOWE, IRINGA
NAIBU gavana wa benki
kuu Tanzania Dkt. Bernard Kibesse kesho jumamosi asubuhi anatarajia
kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa tawi la benki ya MUCOBA PLC tawi la
Iringa mjini liloko katika jengo la Motto Family.
Akizungumza
na mwanahabari ,Mkurugenzi wa benki hiyo, Philipo Nshokigwa alisema
kuwa maandalizi ya uzinduzi wa benki hiyo siku ya kesho yamekwisha
kamilika na kinachosubiriwa ni uzinduzi wa tawi hilo ambapo limehamia
jengo jingine la Motto Family kutoka jengo la Imucu ilipokuwepo awali.
Nshokigwa ametoa wito
kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kushuhudia uzinduzi huo ambapo
wananchi wanaruhusiwa kufungua akaunti kwenye benki hiyo wakati wa
shughuli za uzinduzi zikiendelea.
Alisema kuwa uzinduzi
wa tawi hilo unafanyika kuweza kuendeleza fursa za kiuchumi kwa
wananchi wa mkoa wa Iringa na mikoa jirani hivyo kurahisisha uwekaji wa
kifedha na kukopa kutoka benki hiyo.
Alisema kuwa benki ya
Muccoba ina matawi ndani ya wilaya ya Mufindi na wilaya ya Iringa vijiji
katika jimbo la Ismani ambapo hifadhi ya taifa ya Ruaha ipo hivyo
wanakusudia kupeleka tawi katika eneo la Ruaha ili kuwa karibu zaidi na
watalii ambao wamekuwa wakiongezeka kwa lengo la kuwarahishia zaidi
huduma za kifedha kwa kutumia benki ya MUCCOBA PLC.
Nshokigwa alisema
kuwa kwa kupitia fursa zilizoko mkoa wa Iringa za kiuchumi benki hiyo
imeona vyema kuwasogezea huduma wateja wao kuanzishia mikopo mbalimbali
ikiwemo ya elimu,biashara, watoto na akaunti maalum ambazo zinafanya
kazi katika benki hiyo
Alisema kama
anavyosema Mhe Rais Magufuli anataka wananchi wake wawe na raha
kutokanana na fursa zote zinazopelekea kubadilisha maisha yao, hivyo
kupitia Benki hiyo ipo kuwasaidia wananchi katika kufikia dhana ya
uchumi wa viwanda kwa kusaidia kuongeza dhamana ya mikopo wanayoitaka
katika mabenki.
Amewashauri
wajasiriamali wadogo na wa kati kuzitumia vema fursa mbalimbali za
mikopo kwa wafanyabiashara zilizopo ndani ya Benki ya Muccoba Plc ili
kukuza biashara zao kwa lengo la kukuza kipato cha mmoja mmoja na nchi
kwa ujumla.
NAIBU GAVANA BOT KUZINDUA TAWI LA MUCOBA PLC KESHO IRINGA MJINI
Jengo ambalo benki ya Mucoba Plc ipo na kufanyika uzinduzi wake siku ya kesho iringa mjini.
……………………………………………………………………….
NA DENIS MLOWE, IRINGA
NAIBU gavana wa benki
kuu Tanzania Dkt. Bernard Kibesse kesho jumamosi asubuhi anatarajia
kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa tawi la benki ya MUCOBA PLC tawi la
Iringa mjini liloko katika jengo la Motto Family.
Akizungumza
na mwanahabari ,Mkurugenzi wa benki hiyo, Philipo Nshokigwa alisema
kuwa maandalizi ya uzinduzi wa benki hiyo siku ya kesho yamekwisha
kamilika na kinachosubiriwa ni uzinduzi wa tawi hilo ambapo limehamia
jengo jingine la Motto Family kutoka jengo la Imucu ilipokuwepo awali.
Nshokigwa ametoa wito
kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kushuhudia uzinduzi huo ambapo
wananchi wanaruhusiwa kufungua akaunti kwenye benki hiyo wakati wa
shughuli za uzinduzi zikiendelea.
Alisema kuwa uzinduzi
wa tawi hilo unafanyika kuweza kuendeleza fursa za kiuchumi kwa
wananchi wa mkoa wa Iringa na mikoa jirani hivyo kurahisisha uwekaji wa
kifedha na kukopa kutoka benki hiyo.
Alisema kuwa benki ya
Muccoba ina matawi ndani ya wilaya ya Mufindi na wilaya ya Iringa vijiji
katika jimbo la Ismani ambapo hifadhi ya taifa ya Ruaha ipo hivyo
wanakusudia kupeleka tawi katika eneo la Ruaha ili kuwa karibu zaidi na
watalii ambao wamekuwa wakiongezeka kwa lengo la kuwarahishia zaidi
huduma za kifedha kwa kutumia benki ya MUCCOBA PLC.
Nshokigwa alisema
kuwa kwa kupitia fursa zilizoko mkoa wa Iringa za kiuchumi benki hiyo
imeona vyema kuwasogezea huduma wateja wao kuanzishia mikopo mbalimbali
ikiwemo ya elimu,biashara, watoto na akaunti maalum ambazo zinafanya
kazi katika benki hiyo
Alisema kama
anavyosema Mhe Rais Magufuli anataka wananchi wake wawe na raha
kutokanana na fursa zote zinazopelekea kubadilisha maisha yao, hivyo
kupitia Benki hiyo ipo kuwasaidia wananchi katika kufikia dhana ya
uchumi wa viwanda kwa kusaidia kuongeza dhamana ya mikopo wanayoitaka
katika mabenki.
Amewashauri
wajasiriamali wadogo na wa kati kuzitumia vema fursa mbalimbali za
mikopo kwa wafanyabiashara zilizopo ndani ya Benki ya Muccoba Plc ili
kukuza biashara zao kwa lengo la kukuza kipato cha mmoja mmoja na nchi
kwa ujumla.
No comments :
Post a Comment