Friday, October 9, 2020

KATIBU MKUU MWALUKO AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA UMOJA WA ULAYA, NCHINI TANZANIA.

Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Uwekezaji), Dorothy Mwaluko akielezea masuala ya uboreshwaji wa mazingira ya uwekezaji nchini kwa Balozi wa Umoja wa Ulaya Nchini Tanzania Mhe. Manfredo Fanti alipomtembelea na kufanya mazungumzo katika Ofisi yake iliyopo Mtaa wa Relini Jijini Dodoma, walikutana hii leo Oktoba 09, 2020.

Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Uwekezaji), Dorothy Mwaluko akielezea masuala ya uwekezaji nchini kwa Balozi wa Umoja wa Ulaya Nchini Tanzania Mhe. Manfredo Fanti pamoja na Mkuu wa Idara ya Maendeleo na Mahusiano wa Umoja huo, Cedric Merel walipomtembelea na kufanya mazungumzo katika Ofisi yake iliyopo Mtaa wa Relini Jijini Dodoma.

Balozi wa Umoja wa Ulaya Nchini Tanzania Mhe. Manfredo Fanti akieleza jambo kwa Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Uwekezaji), Dorothy Mwaluko alipomtembelea na kufanya nae mazungumzo kuhusu masuala ya uwekezaji nchini.

Mkuu wa Idara ya Maendeleo na Mahusiano wa Umoja wa Ulaya Bw. Cedric Merel akiuliza jambo kwa Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Uwekezaji), Dorothy Mwaluko wakati wa mazungumzo hayo.

Mkuu wa Idara ya Maendeleo na Mahusiano wa Umoja wa Ulaya Bw. Cedric Merel akiuliza jambo Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Uwekezaji), Dorothy Mwaluko walipomtembelea na kufanya mazungumzo kuhusu masuala ya uwekezaji nchini, Mazungumzo hayo yalifanyika katika ofisi zake Jijini Dodoma.Wa kwanza kushoto ni Mchumi Idara ya Uwekezaji, Bi. Biveline Mshumbusi akifuatilia kikao hicho.

Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Uwekezaji), Dorothy Mwaluko akiteta jambo na Balozi wa Umoja wa Ulaya Nchini Tanzania Mhe. Manfredo Fanti mara baada ya kumaliza mazungumzo yao hii leo Oktoba 09, 2020 Jijini Dodoma.

(PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU)

 

No comments :

Post a Comment