Saturday, September 5, 2020

WANAOTAKA KUJIUNGA NA ELIMU YA JUU WATAKIWA KUFANYA UAMUZI NA UCHAGUZI SAHIHI-TCU


Mwenyekiti wa Tume ya Vyuo Vikuu nchini, Profesa Mayunga Nkunya  akizungumza wakati wa kufunga  maonesho ya vyuo vikuu yanayomalizika leo Septemba 5, katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo Septemba. Maonyesho hayo yakifanyika kwa siku sita ambapo vyuo na wadau mbali mbali wameshiriki
Katibu Mtendaji wa TCU , Profesa Charles  Kihampa akizungumza wakati wa kufunga maonesho ya siku sita ya vyuo vikuu yanayomalizika leo Septemba 5, 2020 katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Profesa Mayunga Nkunya akikagua banda la Chuo Kikuu Muhimbili kabla ya kufunga maonyesho ya 15 ya vyuo vikuu nchini, yanayimalizika leo katika viwanja vya Mnazi mmoja jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wadau wa elimu ya wajuu na washirik wa vyuo vikuu wakifuatilia hotuba ya Profesa Mayunga Nkunya ya kufunga maonyesho ya 15 ya vyuo vikuu nchini, yanayomalizika leo katika viwanja vya Mnazi Mmoja  Jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mtendaji wa Global Education Link, Abdullmalik Mollel akizungumza wakati wa kufunga  Maonesho ya vyuo vikuu yanayomalizika leo jijini Dar es Salaam.
 Na Karama Kenyunko Michuzi TV. 
TUME ya vyuo vikuu (TCU), nchini imewataka wale wote wanaotegeme kujiunga na
elimu juu kufanya maamuzi na uchaguzi sahihi wakati wakiomba udahili kwenye vyuo vya elimu ya juu hapa nchini ili pindi wamalizapo masomo yao waweze kuhimili soko la ajira.
Pia vyuo hivyo vya elimu ya juu vimeshauriwa kutoa elimu bora ili kuzalisha wahitimu mahili, weledi wabunifu na wenye uwezo wa kutatua changamoto za Jamii, watakaoweza kuhimili ushindani katika soko la ajira kitaifa, Kikanda na kimataifa. 
Mwenyekiti wa Tume hiyo, Profesa Mayunga Nkunya ameyasema hayo leo Septemba 5, 2020 wakati akifunga maonesho ya 15 ya vyuo vikuu yaliyokuwa yakifanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Amesema serikali imeendelea kuweka kipaumbele maboresho ya elimu nchini na kupanua wigo na fursa za masomo kwa watanzania na katika ngazi zote za elimu ikiwemo ya elimu ya juu.
"Natoa wito kwa Taasisi zote nchini kuendelea kuunga mkono juhudi za serikali za kuongeza fursa za masomo kwa Watanzania wengi zaidi lakini bila kuathiri ubora" amesema Nkunya.
Ameongeza kuwa, ili kuweza kupata elimu bora inayokidhi mahitaji ya Taifa, kikanda na Kimataifa Taasisi zote za elimu ya juu zinapaswa kusimamiwa ili kuhakikisha zinakuwa na mifumo imara ya udhibiti ubora inayolenga kuzalisha wataalamu wanaohitajia ambapo ili kufikia azma hiyo vyuo vinahitaji kuwa na viongozi imara, bora, wenye mtazamo chanya, weledi na wenye maarifa ya kutosha kusimamia sera na miongozo mbali mbali ya elimu ya juu nchini kwa kuzingatia mabadiriko katika sekta ya elimu ya juu yanayotokea nchini na duniani kote.
" Udahili wa elimu ya juu nchini bado uko chini sana.., katika nchi za Afrika miaka miwili iliyopita udahili ulikuwa kama asilimia nane kwa wale wanaokidhi vigezo lakini sisi hapa ni asilimia nne tu  bado tuko chini sana... hatuna budi kuongeza bidii ili kuweza kupanua wigo wa udahili wa wanafunzi katika vyuo vikuu lakini tukizingatia ubora amesema Profesa Nkunya.
Ameongeza, hivi karibuni nchi yetu iliingia kwenye orodha ya nchi zenye uchumi wa kati hayo mafanikio ambayo kila mmoja wetu anapaswa kujivunia, ni hukumu letu kila.mmojankuchukua hatua.
Pia Profesa Nkunya ametoa wito kwa viongozi wa vyuo vya elimu ha juu nchini kusimamia kwa ukaribu na umakini mchakato mzima wa udahili kwa wanafunzi wa elimu ya juu kwa mwaka wa masomo wa 2020, 2021 kwa kuzingatia miongozo iliyowekwa ili kuondoa usumbufu usiokuwa wa lazima kwa waombaji, wazazi, walezi wafadhili na wadau wengine wa elimu ya juu.
Kwa upande wake, Katibu Mtendaji wa TCU, Charles  Kihampa amesema katika maonyeshao hayo ya siku sita,  jumla ya Taasisi 67 zimeshiriki ziwemo taasisi za mafunzo ya ngazi ya elimu ya juu 58, mabaraza ya uthibiti ubora mawili,  wakala na Taasisi nyingine za serikali zilikuwa na bodi moja ya usajili wa wataalamu. Taasisi za Sayansi techonojia na utafiti mbili na Taasisi za huduma za kifedha mbili.
Amesema, malengo ya maonyeshao hayo yalikuwa ni pamoja na kutoa fursa kwa Taasisi zinazoshiriki kujitangaza kwa kuonesha huduma na kazi mbali mbali wanazofanya na mchango wao katika ustawi wa elimu ya juu kwa mustakabali wa Maendeleo ya Sayansi na Teknolojia na manufaa yake kiuchumi na kijamii.
Amesema pia Maonesho yanawapa fursa wananchi, wafanyabiashara na wenye viwanda kuweza kujifunza na kuanzisha ushirikiano wa kujenga na kuimarisha mahusiano baina ya Taasisi hizo za elimu ya juu.
Amesema, mpaka kufikia leo hii jumla ya wanafunzi 33969 wanaotaka kujiunga na elimu ya juu wameishatuma maombi yao ya kujiunga na shahada ya kwanza katika vyuo mbali mbali na pia amewashauri wanaotaka kujiunga katika degree za awali iuendelea kutuma maombi yao katika dirisha hilo  kwanza ambalo linatarajiwa kufunga Septemba 25, mwaka huu na siyo kusubiri mpaka wanapokaribia kufika mwisho ndio waanze kuangaika.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Global Education Link, Abdullmalik Mollel akizungumza kwa niaba ya washiriki, amevushauri vyuo vikuu vya ndani hapa nchini kuweka viwango vya kumtambua ama kumruhusu mwalimu aajiriwe kujikita kwenye uwezo wa msingi (competent base) na siyo ufaulu wa GPA.
"Tunaona sisi vyuo vikuu vya nje, mwalimu anaweza kuwa na GPA ndogo lakini output ya kijana wake ikawa ni nzuri sana ni vema ukatengenezwa mfumo ili vyuo vikuu vyetu  vya ndani viweze kuwa na idadi kubwa ya wanafunzi inayoendana na idadi kubwa pia ya wahadhiri katika vyuo hivyo", amesema Mollel
Ameongeza, vyuo vinapowekwa vigezo vya juu sana katika kumdahili mwalimu inawezekana tukajitengenezea ushindani mkubwa na kutengeneza uhitaji kwa wale wachache waliopo na vyuo vikashindwa kupanuka kwa haraka. 
Mollel pia amevipongeza vyuo vikuu vyote na Taasisi za elimu ambazo zimefanya udahili wa moja kwa moja viwanjani hapo kwa kuweza kuwapa wanafunzi majibu ya moja kwa moja.

No comments :

Post a Comment