Thursday, August 13, 2020

WAZIRI MHAGAMA AAGIZA UONGOZI WA KIWANDA CHA KUCHAKATA BIDHAA ZA NGOZI CHA KARANGA KUANZA KUTAFUTA MASOKO


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na Wasimamizi wa mradi wa Ujenzi wa Kiwanda cha bidhaa za ngozi cha Karanga alipotembelea kiwanda hicho kukagua maendeleo ya ujenzi. Kushoto ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Bw. Andrew Massawe.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Bw. Andrew Massawe akieleza jambo wakati wa kikao kifupi cha upokeaji wa taarifa ya utekelezaji wa mradi wa Ujenzi wa Kiwanda cha bidhaa za ngozi cha Karanga.

Mkurungenzi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), Bw. Hosea Kashimba akitoa taarifa fupi kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama mara baada ya kuwasili kiwandani hapo kwa ajili ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi huo. Wa kwanza Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda hicho Mhandisi Masud Omar.

Muonekano wa baadhi ya Majengo ya Kiwanda hicho yaliyojegwa katika awamu ya kwanza (LOT 1) yakiwa yamekamilika.

Sehemu ya Mitambo ambayo itasimikwa katika majengo yaliyokamilika katika awamu ya kwanza ya ujenzi wa kiwanda cha Karanga kilichopo Mkoani Kilimanjaro.

Baadhi ya Mafundi wakisuka ndondo katika maeneo eneo moja wapo la awamu ya pili ya ujenzi ya kiwanda hicho cha kuchakata Ngozi kilichopo Moshi, Mkoani Kilimanjaro.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Bw. Andrew Massawe (wa pili kutoka kushoto) akiwa ameambatana pamoja na Wasimamizi wa mradi wa ujenzi wa kiwanda cha bidhaa za ngozi alipokuwa akigagua maendeleo ya mradi huo uliopo Moshi, Mkoani Kilimanjaro. Kushoto ni Mkurungenzi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), Bw. Hosea Kashimba.

Mratibu Msaidizi ambaye pia ni Mhandisi wa Umeme, Paul Kiweri (kulia) akifafanua jambo kwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Bw. Andrew Massawe (wa nne kutoka kulia) walipotembelea eneo la usambazaji mifumo ya umeme “Power House” katika kiwanda hicho.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Bw. Andrew Massawe (katikati) akitoa maelekezo kwa wasimamizi wa mradi wa ujenzi wa kiwanda cha bidhaa za ngozi alipokuwa akigagua maendeleo ya mradi huo uliopo Moshi, Mkoani Kilimanjaro.

PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU

(KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU)

OWM – KVAU

 

No comments :

Post a Comment