Waziri wa Fedha, Dkt. Philip
Mpango akipokea mfano wa hundi ya gawio la shilingi bilioni 9.3 kutoka
kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Benki yah CRDB, Dkt. Ally Laay
(watatu kushoto) kutokana na uwekezaji wa Serikali ndani ya benki hiyo
kupitia Mfuko wa Uwekezaji wa DANIDA kwa kushirikiana na Serikali ya
Denmark. Waziri Mpango leo amepokea jumla ya gawio la shilingi bilioni
17 kutoka Benki ya CRDB ikiwa ni gawio kutokana na uwekezaji wa Serikali
kuu, taasisi na mashirika yake. Wengine pichani ni Waziri wa TAMISEMI,
Suleiman Jaffo (wanne kushoto), Waziri wa Sera, Bunge, Vijana, Ajira na
Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama (watatu kulia), Balozi wa Denmark Nchini,
Mette Dissing-Spandet (wapili kulia), Msajili wa Hazina, Athman
Mbuttuka (wakwanza kulia), Makamu Mwenyekiti wa Bodi Benki ya CRDB,
Prof. Neema Mori (wakwanza kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya
CRDB, Abdulmajid Nsekela.
Waziri wa Sera, Bunge, Vijana,
Ajira na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama (wapili kulia) akipokea gawio la
shilingi bilioni 5.8 kutoka Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Benki ya
CRDB, Dkt. Ally Laay (wapili kushoto) na kumkabidhi Mkurugenzi Mkuu wa
Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa PSSSF, Hosea Kashimba (wakwanza kulia),
kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela.
Benki ya CRDB leo imekabidhi jumla ya gawio la shilingi bilioni 17
kutokana na uwekezaji wa Serikali kuu, taasisi na mashirika yake.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais
Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa,(TAMISEMI) Selemani Jafo akipokea
gawio kutokana na uwekezaji wa Halmashauri za Mbinga, Lindi, Shinyanga,
Mufindi, Chunya na Rungwe leo jijini Dodoma
Waziri wa Fedha, Dkt. Philip Mpango akitoa hotuba yake
katika hafla fupi ya kupokea jumla ya gawio la shilingi bilioni 17
kutoka Benki ya CRDB ikiwa ni gawio kutokana na uwekezaji wa Serikali
kuu, taasisi na mashirika yake, iliyofanyika leo kwenye Ukumbi wa
Hazina, jijini Dodoma leo.
Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Ajira, Vijana
na wenye Ulemavu, Jenista Mhagama akisisitiza jambo wakati wa hafla
fupi ya kupokea jumla ya gawio la shilingi bilioni 17 kutoka Benki ya
CRDB ikiwa ni gawio kutokana na uwekezaji wa Serikali kuu, taasisi na
mashirika yake, iliyofanyika leo kwenye Ukumbi wa Hazina, jijini Dodoma
leo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za
Mitaa,(TAMISEMI) Selemani Jafo akizungumza wakati wa hafla fupi ya
kupokea jumla ya gawio la shilingi bilioni 17 kutoka Benki ya CRDB ikiwa
ni gawio kutokana na uwekezaji wa Serikali kuu, taasisi na mashirika
yake, iliyofanyika leo kwenye Ukumbi wa Hazina, jijini Dodoma leo.
Balozi wa Denmark Tanzania,
Mette Dissing-Spandet,akizungumza wakati wa hafla fupi ya kupokea jumla
ya gawio la shilingi bilioni 17 kutoka Benki ya CRDB ikiwa ni gawio
kutokana na uwekezaji wa Serikali kuu, taasisi na mashirika yake,
iliyofanyika leo kwenye Ukumbi wa Hazina, jijini Dodoma leo.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt.
Ally Laay akitoa hotuba yake katika hafla fupi ya kukabidhi hundi zenye
jumla ya gawio la shilingi bilioni 17 kutoka Benki ya CRDB ikiwa ni
gawio kutokana na uwekezaji wa Serikali kuu, taasisi na mashirika yake,
iliyofanyika leo kwenye Ukumbi wa Hazina, jijini Dodoma leo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela
akitoa hotuba yake katika hafla fupi ya kukabidhi hundi zenye jumla ya
gawio la shilingi bilioni 17 kutoka Benki ya CRDB ikiwa ni gawio
kutokana na uwekezaji wa Serikali kuu, taasisi na mashirika yake,
iliyofanyika leo kwenye Ukumbi wa Hazina, jijini Dodoma leo.
Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Benki ya CRDB, Tully Esther
Mwambapa akitoa taarifa kwenye hafla fupi ya kukabidhi hundi zenye jumla
ya gawio la shilingi bilioni 17 kutoka Benki ya CRDB ikiwa ni gawio
kutokana na uwekezaji wa Serikali kuu, taasisi na mashirika yake,
iliyofanyika leo kwenye Ukumbi wa Hazina, jijini Dodoma leo.
Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB,
Prof. Neema Mori akitoa shukrani za Bodi kwa Serikali baada ya katika
hafla fupi ya kukabidhi hundi zenye jumla ya gawio la shilingi bilioni
17 kutoka Benki ya CRDB ikiwa ni gawio kutokana na uwekezaji wa Serikali
kuu, taasisi na mashirika yake, iliyofanyika leo kwenye Ukumbi wa
Hazina, jijini Dodoma leo.
Sehemu ya wadau wakisikiliza hotuba ya Waziri wa Fedha,
Dkt. Philip Mpango wakati wa kupokea jumla ya gawio la shilingi bilioni
17 kutoka Benki ya CRDB ikiwa ni gawio kutokana na uwekezaji wa
Serikali kuu, taasisi na mashirika yake, iliyofanyika leo kwenye Ukumbi
wa Hazina, jijini Dodoma leo.
Waziri wa Fedha, Dkt. Philip Mpango akiwa katika picha ya
pamoja na waandishi wa habari mara baada ya kupokea jumla ya gawio la
shilingi bilioni 17 kutoka Benki ya CRDB ikiwa ni gawio kutokana na
uwekezaji wa Serikali kuu, taasisi na mashirika yake, iliyofanyika leo
kwenye Ukumbi wa Hazina, jijini Dodoma leo.
…………………………………………………………………….
Waziri wa Fedha na Mipango Dokta Philip Mpango amepokea
gawio la shilingi bilioni 17 linalotokana na uwekezaji wa Serikali ndani
ya Benki ya CRDB kutoka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki
ya CRDB, Dkt. Ally Laay.
Makabidhiano hayo ya hundi kifani yalifanyika katika ukumbi
wa Kambarage, Wizara ya Fedha na Mipango Dodoma na kuhudhuriwa na
baadhi ya mawaziri na viongozi mbalimbali wa taasisi na mashirika ya
umma yenye hisa ndani ya Benki ya CRDB na Menejementi ya Benki ya CRDB.
Akizungumza katika hafla hiyo Dkt. Mpango aliipongeza Benki
hiyo kwa kutoa gawio kwa Serikali na kwa kupata faida katika biashara
yake katika kipindi cha mwaka 2019/20 ambayo yamepelekea kuongezeka kwa
gawio kwa Wanahisa ikiwamo Serikali.
Katika mwaka wa fedha 2018/2019 Benki ya CRDB ilitoa gawio
la shilingi bilioni 10 kwa Serikali na mwaka 2019/2020 imetoa gawio la
shilingi bilioni 17 jambo ambalo Dkt. Mpango alisema nimapinduzi makubwa
katika utendaji wa benki hiyo.
Mhe.Mpango amesema kuwa umuhimu wa ushiriki wa taasisi za
fedha katika maendeleo ya taifa, Dkt. Mpango aliipongeza Benki ya CRDB
kwa kupunguza riba katika mikopo kutoka asilimia 24 kufikia wastani wa
asilimia 18 na 14 ili kuchochea shughuli za maendeleo nchini.
“Niwapongeze kwa kupunguza riba katika mikopo, hiki kimekuwa kilio cha
muda mrefu cha Serikali kwa mabenki nchini, niyasihi mabenki mengine
kufuata nyayo hizi za Benki ya CRDB,” alisema Dkt. Mpango.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt.
Ally Laay, alisema kuwa gawio hilo ni sehemu ya faida ya shilingi
bilioni 120.1 baada ya kodi ambayo Benki ya CRDB na kampuni zake tanzu
imeipata katika mwaka wa fedha 2019/2020 na kuahidi kuwa Benki hiyo
itaendelea kutoa huduma bora ili kukidhi mahitaji ya wanahisa wake na
wananchi kwa ujumla.
“Katika Mkutano wa Wanahisa uliofanyika kidijitali mwezi
Juni mwaka huu, Wanahisa wa Benki ya CRDB walipitisha kwa pamoja gawio
la shilingi 17 kwa hisa ikiwa ni ongezeko la asilimia 112.5 na hivyo
kufanya gawio la mwaka huu kufikia jumla ya shilingi bilioni 44.4,”
aliongezea Dkt. Laay.
Aidha, Dkt. Laay aliipongeza Serikali ya Awamu ya Tano ya
Dkt. John Pombe Magufuli kwa utendaji mzuri ambao umeiwezesha Benki ya
CRDB kuendelea kutekeleza majukumu yake kwa weledi na kuahidi kuendelea
kushirikiana nayo ili kukuza uchumi wa nchi.
Awali Mkurugenzi Mtendaji wa
Benki ya CRDB Abdulmajid Nsekela alimhakikishia Dokta Mpango kuwa Benki
ya CRDB kupitia kauli mbiu yake ya “Tupo Tayari” itaendelea kushirikiana
na Serikali katika kuboresha upatikanaji wa huduma za kifedha nchini
huku akielezea kuwa benki hiyo sasa hivi imejikita zaidi kwenye
uwekezaji wa mifumo ya kidijitali ya kutolea huduma kama CRDB Wakala,
SimBanking, SimAccount na Internet banking ambayo humsaidia mteja kupata
huduma kwa urahisi, unafuu na haraka.
Akipokea gawio kutokana na
uwekezaji wa Halmashauri za Mbinga, Lindi, Shinyanga, Mufindi, Chunya na
Rungwe, Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI, Suleiman Jaffo amezihimiza
halmashauri nyingine nchini kuwekeza katika hisa ili kupanua wigo wa
mapato katika halmashauri zao.
Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu
Sera, Bunge, Ajira, Vijana na wenye Ulemavu, Jenista Mhagama alipongeza
mifuko ya jamii ya PSSSF, NSSF na ZSSF kwa uwekezaji ndani ya Benki ya
CRDB huku akiwataka viongozi wa mifuko hiyo kutumia gawio walilopata
kuboresha utendaji kazi ili kunufaisha wanachama wa mifuko hiyo.
Kwa upande wake Balozi wa
Denmark Tanzania, Mette Dissing-Spandet amesema Serikali ya Denamark
inajivunia kwa uwekezaji ulioufanya ndani ya Benki ya CRDB kwa
kushirikiana na Serikali ya Tanzania kupitia Mfuko wa Uwekezaji wa
DANIDA huku akibainisha kwa pamoja Serikali hizo zimekubaliana kuelekeza
gawio hilo katika kuboresha sekta ya afya nchini.
Serikali ndio mwanahisa mkubwa
ndani ya Benki ya CRDB kutokana na kuwa na umiliki wa asilimia 21
kupitia mfuko wa uwekezaji wa DANIDA kushirikiana na Serikali ya
Denmark, huku taasisi na mashirika ya umma yakiwa na umiliki wa hisa za
asilimia 17.1.
No comments :
Post a Comment