Friday, July 10, 2020

TUME YA MADINI YAVUKA LENGO LA UKUSANYAJI WA MAPATO


 
Kifaa cha Kudetect Madini kwenye Miamba  Bidhaa ya Madini yaliyotoa vitu vya thamani
NA EMMANUEL MBATILO
Tume ya Madini imeweza kuvuka lengo walilopewa la ukusanyaji wa mapato kwani mwaka 2019-2020 walipewa lengo la kukusanya Bilioni 470 hivyo wao wamevuka na kukusanya Bilioni 528.2.
Akizungumza katika banda la tume hiyo katika Viwanja vya Maonesho vya Mwalimu Nyerere Jijini Dar Es Salaam, Mtakwimu wa Tume ya Madini Bw.Azihar Kashakara amesema kuwa
tume imekuwa na mchango mkubwa katika pato la Serikali hadi kufikia nchi kwenye uchumi wa kati.
“Kupitia Tume ya Madini kuweza kukusanya kwa makini tozo mbalimbali zinazotokana na shughuli mbalimbali za madini zimeweza kusaidia kuwa na mchango mkubwa nchi kufikia uchumi wa kati”.Amesema Bw.Kashakara.
Kwa upande wake Meneja Habari na Mawasiliano-Tume ya Madini Bw.Greyson Mwase amesema katika Maonesho ya mwaka huu Tume ya Madini imeweza kushirikisha wachimbaji wadogo na waongezaji thamani madini na wametumika kama mfano wa kuwahamasisha wananchi ambao wanania ya kuingia kwenye uchimbaji mdogo wa madini.
“Maonesho yamekuwa na manufaa na tumejiandaa kikamilifu na tutaendelea kushiriki forum mbalimbali kwaajili ya kuhakikisha wawekezaji kutoka nje ya nchi wanakuja kuwekeza hapa nchini katika sekta ya Madini na hasa ukizingatia nchi yetu tumeingia kwenye nchi yenye kipata cha kati na sisi tutaendelea kufana vizuri zaidi huku tukihakikisha sekta ya madini inakuwa na mchango mkubwa”. Amesema Bw.Mwase.
Aidha Bw.Mwase amesema wananchi wengi wamekuwa wakija kuulizia kuhusiana na namna gani wanaweza kujiingiza kwenye shughuli za uchimbaji wa madini pamoja na taratibu za kupata leseni.
Hata hivyo Bw.Mwase amesema wengi wamesikia masoko ya madini yaliyoanzishwa hivyo basi wengi wameonesha nia ya kufanya biashara ya madini kutumia mfumo wa masoko ulioanzishwa.
“Wananchi wameweza kuelimika hivyo kupitia soko la madini litaenelea kukua zaidi kutokana wengi kuwa na uelewa mkubwa namna ya kuendesha biashara ya Madini”.Amesema Bw.Mwase.

No comments :

Post a Comment