Afisa
Uhusiano Mwandamizi wa Chuo cha Uhasibu Arusha Bi. Sarah Goroi(kulia)
akitoa maelezo kwa Mkuu wa Jeshi la Anga Meja Jenerali George William
Ingram(kushoto), kuhusu kozi mpya zinazotarajiwa kuanza kufundishwa na
chuo hicho mwezi Oktoba, 2020 wakati alipotembelea banda la Wizara ya
Fedha na Mipango pamoja na Taasisi zake katika Maonesho ya 44 ya
Kimataifa ya Biashara jijini Dar es Salaam.
Afisa Udahili wa Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) Sekunda Titus(kulia) akitoa ufafanuzi kuhusu usajili kwa njia ya mtandao na kozi mpya zinazotarajiwa kuanza kufundishwa na chuo hicho mwezi Oktoba, 2020 kwa mwananchi aliyetembelea katika banda la Chuo hicho katika Maonesho ya 44 ya Kimataifa ya Biashara jijini Dar es Salaam.
Afisa Udahili wa Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) Sekunda Titus(kulia) akitoa ufafanuzi wa kozi zilizopo na kozi mpya zinazotarajiwa kuanza kufundishwa na chuo hicho mwezi Oktoba, 2020 katika chuo hicho kwa mwananchi aliyetembelea katika banda la Chuo hicho katika Maonesho ya 44 ya Kimataifa ya Biashara jijini Dar es Salaam.
Afisa Uhusiano Mwandamizi wa Chuo cha Uhasibu Arusha Bi. Sarah Goroi, akitoa maelezo
kwa wananchi kuhusu kozi mpya zinazotarajiwa kuanza kufundishwa na chuo
hicho mwezi Oktoba, 2020 waliotembelea katika banda hilo katika
Maonesho ya 44 ya Kimataifa ya Biashara jijini Dar es Salaam.
No comments :
Post a Comment