*******************************
NA MWAMVUA MWINYI,CHALINZE
MKUU wa Wilaya ya
Bagamoyo Mkoa wa Pwani Zaynabu Kawawa, ameikabidhi Halmashauri ya
Chalinze ,vitambulisho vya Mjasiriamali vipatavyo 10,106 na kuagiza
wasibughudhiwe.
Aidha amewaonya Watendaji wataokwamisha zoezi la usambazaji wa vitambulisho maalumu kwa ajili ya wajasiriamali.
Katika hafla fupi ya
makabidhiano hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa shule ya
Sekondari Lugoba, Kawawa alisema, vitambulisho hivyo vilivyotolewa na
Rais John Magufuli kwa wajasiriamali wadogo, vinalenga kuwaondolea adha
walengwa hao ambapo kupitia mpango huo Serikali kupitia Mamlaka ya
kukusanya Mapato TRA itakuwa imekusanya pesa za kutosha.
Akizungumza kabla ya
kukabidhi vitambulisho hivyo, Kawawa alibainisha,kwa mwaka huu wilaya
hiyo yenye Halmashauri mbili ya Chalinze zimepata vitambulisho 17,000
ikiwemo Chalinze wamepata zaidi ya 10,106 na Bagamoyo ni 6,891.
Hata hivyo,alisema hatokuwa na msamaha kwa atayeonekana kuwa kikwazo kwenye zoezi hilo.
Kaimu Mkurugenzi wa halmashauri hiyo ,Zaynabu Makwinya alieleza, wamejiandaa kuhahakisha zoezi litamwenda vizuri.
Alisema, wamejipanga
vizuri kuhakikisha kwamba vitambulisho hivyo vinauzwa na hadi Juni 5
vitakuwa vimemalizika, huku akieleza kuwa kuna gari maalumu linalotumika
kwa ajili ya zoezi hilo.
“Kwa Watendaji ambao
watamaliza mapema vitambulisho vyao watawasiliana na Maofisa Tarafa, ili
tujulishwe tumwambie ofisa Ushirika awapelekee waendelee na zoezi la
uuzwaji wa vitambulisho hivyo,” alisema Makwinya.
Kaimu Ofisa Mfawidhi
wa TRA Kanda ya Chalinze David Tawa alieleza ,zoezi hilo ni muhimu
kwakuwa wajasiriamali wanaingia katika mfumo wakutambulika.
No comments :
Post a Comment