Naibu Waziri, Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary
Mwanjelwa (Mb) akizungumza na Mnufaika wa Mpango wa Kunusuru Kaya
Maskini Bibi Rozena Bilia Mwambogo alipomtembelea mnufaika huyo kijiji
cha Mapogoro wilayani Chunya wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Waziri
huyo yenye lengo la kukagua utekelezaji wa mpango wa TASAF mkoani Mbeya.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary
Mwanjelwa (Mb) na Mnufaika wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini, Bibi
Rozena Bilia Mwambogo wakielekea kushuhudia banda la nguruwe wanaofugwa
na mnufaika huyo kutokana na ruzuku ya TASAF.
Banda la Nguruwe wanaofugwa na Bibi Rozena Mwambogo ambao amewanunua kupia ruzuku ya Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini (TASAF).
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary
Mwanjelwa (Mb) akizungumza na mgonjwa, Mzee Gidison Mwayiyi ambae
anauguzwa na mnufaika wa TASAF Bibi Rozena Mwambogo alipomtembelea
mnufaika huyo katika kijiji cha Mapogoro wilayani Chunya wakati wa ziara
ya kikazi ya Naibu Waziri huyo yenye lengo la kukagua utekelezaji wa
mpango wa TASAF mkoani Mbeya.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Mary Mwanjelwa
(Mb) akimfariji mgonjwa, Mzee Gidison Mwayiyi ambae anauguzwa na
mnufaika wa TASAF Bibi Rozena Mwambogo alipomtembelea mnufaika huyo
katika kijiji cha Mapogoro wilayani Chunya.
……………………………………………………………………………………
Na. James K. Mwanamyoto – Chunya
Bibi mwenye umri wa miaka tisini,
mkazi wa kijiji cha Mapogoro wilayani Chunya ambaye ni
Mnufaika wa
Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini (TASAF) Rozina Bilia Mwambogo,
ameboresha maisha yake kwa kujenga nyumba ya kuishi, kujishughulisha na
kilimo na mazao ya chakula ikiwa ni pamoja na kufuga nguruwe.
Bibi Mwambogo ametoa ushuhuda wa
kuboresha maisha yake kupitia TASAF wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu
Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,
Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) wilayani Chunya yenye lengo la kukagua
Utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini mkoani Mbeya.
Bibi Mwambogo amemueleza Dkt.
Mwanjelwa kuwa, kabla ya kuingizwa kwenye mpango, hali ya maisha yake
ilikuwa chini sana kwani hakuwa na kipato cha kumuwezesha kupata
mahitaji muhimu ya kila siku kama chakula na mavazi.
Bibi Mwambogo ameongeza kuwa,
malengo yake ya baadaye ni kuboresha zaidi maisha yake kwa kuongeza
idadi ya Nguruwe na kuku na kuongeza uzalishaji wa mazao mashambani hasa
ya chakula.
Aidha, Bibi Mwambogo ameishukuru Serikali kwa kuendelea kuwajali wanyonge na kuwasaidia kupitia TASAF.
Kwa upande wake, Dkt. Mwajelwa
amemueleza Bibi Mwambogo kuwa, Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na
Dkt. John Pombe Magufuli inazijali na kuzithamini kaya zote maskini
nchini ndio maana inatoa ruzuku kupitia TASAF, lengo likiwa ni
kuzikwamua katika lindi la umaskini.
Dkt. Mwanjelwa amefafanua kuwa,
ziara yake ya kikazi ya kumtembelea Bibi Mwambogo ni sehemu ya kumuunga
mkono Mhe. Rais, Dkt. John Pombe Magufuli ambaye amejipambanua kwa
vitendo kuwajali wanyonge.
Dkt. Mwanjelwa amempongeza Bibi
Mwambogo kwa kutumia vema ruzuku anayoipata licha ya umri mkubwa alio
nao, na ametoa wito kwa wananchi hususani wanufaika wa TASAF kutumia
vema fedha za miradi ya Serikali kama ilivyokusudiwa.
Uhawilishaji wa fedha kwa kaya
maskini wilayani Chunya ulianza mwezi Julai, 2015 na hadi sasa awamu 23
za malipo zimefanyika ambapo kiasi cha shilingi 7,472,420,000/= za
kitanzania kimetumika kuwapa walengwa ruzuku.
No comments :
Post a Comment