Monday, March 2, 2020

DK. SULEIMAN MISANGO: MAANA YA UKUAJI WA UCHUMI NI ONGEZEKO LA SHUGHULI ZA UZALISHAJI MALI, BIDHAA NA HUDUMA


Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Tafiti za Uchumi BoT, Dkt. Suleiman Misango, akitoa mada kuhusu mapitio ya maendeleo ya uchumi nchini, kikanda na dunia na matarajio kwa mwaka 2020.
………………………………………………
Tunapoongelea kuhusu dhana ya ukuaji wa uchumi maana yake ni ongezeko la shughuli za
uzalishaji mali wa bidhaa na huduma  nchini.
Shughuli hizi zinapokuwa zinaongezeka ina maana kwamba ni ongezeko  kwenye kipato cha mwananchi kwa sababu ni mwananchi  mmoja mmoja  na makampuni ndiyo yanayojishughulisha na shughuli za uzalishaji mali.
Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Tafiti za Uchumi BoT, Dkt. Suleiman Misango ameyasema hayo mara baada ya kuwasilisha mada katika semina ya waandishi wa habari za uchumi na Fedha inayoendelea katika tawi la BoT jijini Arusha
Amesema kwa miaka ya hivi karibuni uchumi wetu umekuwa ukikua kwa asilimia 7 kwa mwaka 2018 na kwa mwaka uliotangulia uchumi wetu ulikuwa kwa asilimia 6.8 na ukichukua wastani wa ukuaji wa uchumi kwa miaka mitano ya nyuma iliyopita kutoka 2018 mpaka 2014   uchumi wetu ulikuwa kwa asilimia  6.7.
Akielezea zaidi Dk Misango amesema uchumi unapokuwa unakuwa ni ongezeko la la kipato na sehemu ya kipato hiki kinachukuliwa na serikali kwa njia ya kodi ambapo serikali inachukua hizi fedha kwa ajili ya matumizi ya serikali.
Amesema katika Matumizi haya fedha hizi ndizo zinazotumika katika shughuli za maendeleo kama vile kujenga miundombinu ya  Barabara, Shule, Reli , Umeme, huduma za afya ,Jamii na shughuli zingine za usimamizi wa  maendeleo kwa  ujumla wake.
Ameongeza kuwa  kutokana na shughuli za uzalishaji mali kuongezeka. Kazi ya BoT ni kuhakikisha kwamba inatoa fedha kulingana na mwenendo wa ukuaji wa uchumi, na kwa kadri uchumi unavyokua BoT inahakikisha kiasi cha fedha kilichopo kwenye uchumi kipo kwenye kiwango kinachohitajika.
Amesema kuwepo kwa fedha mtaani kunategemea shughuli za uzalishaji mali na shughuli za maendeleo kuongezeka kwa sababu BoT inatoa fedha kwenda kwenye uchumi kwa njia kuu mbili  moja inatoa kwa  serikali kwa ajili ya kulipia miradi ya maendeleo na shughuli zingine za usimamizi wa  maendeleo.
“Njia ya pili ni kupitia mabenki kwa sababu mabenki yanashirikiana na BoT katika kufanya shughuli zake za kila siku mabenki hayo yanapohitaji fedha ndiyo Benki Kuu inavyotoa fedha hizo katika uchumi kwa mabeki.
Katika  kipindi cha hivi karibuni mikopo katika mabenki kwenda kwenye sekta binafsi imeongezeka kwa kiasi kikubwa kulingana na matarajio na sisi tunaona bado hili liko ndani ya matarajio yetu”. amesema Dk Misango.
Amesema serikali imekuwa ikifanya shughuli nyingi za miradi ya maendeleo ambapo inatumia fedha nyingi ambazo zinaingia kwenye mzunguko.
Hii dhana ya kusema kwenye mzungukoi hakuna fedha haiko sawa kwa sababu fedha zimekuwa zikiongezeka katika uchumi kutokana na watu wanaoavyofanya  shughuli hizo za kiuchumi na maendeleo.
Ameongeza kuwa kwa siku za hivi karibuni  ongezeko la ujazo wa fedha limekuwa kati ya asilia 8 mpaka 9. Lakini kitu ambacho kimetokea kwenye uchumi ambacho ni muhimu watu wakaelewa ni maendeleo katika mifumo ya malipo.
Mzunguko wa fedha unaenda kwa haraka zaidi unapata fedha unamlipa mtu A. na Mtu A naye anamlipa mwingine kwa hiyo mzunguko unakuwa mkubwa kuliko kiwango kilichokuwa kinatokea zamani,  lakini jambo kubwa hapa ni ule mzunguko wa fedha unatakiwa uuiane na fedha taslimu ambayo inakuwa imetolewa katika shughuli za uchumi.
Dk. Misango anemalizia na kusema ingekuwa mzunguko wa fedha umepungua katika uchumi  lingekuwa jambo gumu sana kusema kuhusu ukuaji wa uchumi ambao tumekuwa tukiusema kila wakati.

No comments :

Post a Comment