Saturday, February 29, 2020

NDITIYE AHITIMISHA KAMPENI YA “SWITCH-ON, MAWASILIANO KWA WOTE” KANDA YA KASKAZINI



Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Nchini, Mh. Atashasta Nditiye (wa pili kushoto) akikata utepe kuashiria Uzinduzi wa Mnara wa Mawasiliano wa TTCL katika kampeni ya  “SWITCH-ON, Mawasiliano kwa wote” katika kijiji cha Irkuishbo wiliyani Kiteto mkoani Manyara.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Nchini, Mh. Atashasta Nditiye (wa pili kushoto) akishangilia pamoja na wananchi wa kijiji cha Irkuishbor, Kiteto Mkoani Manyara mara baada ya kukata utepe ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa Mnara wa Mawasiliano wa TTCL.
…………………………………………………………………………………………..
Na Mwandishi wetu,
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Nchini, Mh. Atashasta Nditiye Ijumaa ya
tarehe 28 Februari, 2020 amehitimisha Kampeni maalum ya Shirika la Mawasiliano Nchini, TTCL ijulikanayo kama “SWITCH-ON, Mawasiliano kwa wote” kwa mikoa ya Ukanda wa Kaskazini mwa Tanzania katika kijiji cha Irkuishbor wilayani Kiteto Mkoani Manyara.
Kampeni hiyo iliyoambatana na zoezi la kuzindua Minara ya Mawasiliano ya Shirika hilo kwa ukanda wa Kaskazini ilianzia Jijini Tanga tarehe 25 Februari, 2020 na kuendelea katika mikoa ya Kilimanjaro, Arusha na kuhitimishwa Mkoani Manyara.
Katika ziara hiyo, Naibu Waziri aliambatana na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano nchini, Bw. Waziri Kindamba, Meneja Uhusiano wa Shirika hilo Bi. Puyo Nzalayaimisi na kupokelewa na viongozi mbalimbali wa ngazi za Mkoa wa Shirika hilo kubwa la Mawasiliano.
Mh. Nditiye alisema Kampeni hii itaendelea sehemu mbalimbali nchini ambazo zina changamoto ya mawasiliano, “Nimeshiriki katika ziara hii ya kampeni ya SWITCN-ON, Mawasiliano kwa wote, ambayo inasimamiwa na TTCL Corporation katika mkoa wa Morogoro, Tanga, Kilimanjaro na Arusha. Nilizindua rasmi kampeni hii katika kambi ya kikosi 121 Mkoani Morogoro Kidugala Sangasanga, baadaye nikazindua Mnara wa Mawasiliano katika kata ya Masalai Muheza Tanga, Kashashi Siha Kilimanjaro, Mundarara Longido Arusha na hatimaye kuhitimisha katika wilaya hii ya Kiteto, Manyara na tutaendelea na zoezi hili Nchi nzima kuweza kuwafikia wananchi wote”.

No comments :

Post a Comment