Sunday, January 12, 2020

SERIKALI YAONYA WANANCHI WANAOJENGA MIJINI BILA KUFUATA UTARATIBUSERIKALI YAONYA WANANCHI WANAOJENGA MIJINI BILA KUFUATA UTARATIBU



Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi aonya wananchi wanaojenga mijini bila kufuata utaratibu. 
Mhe. Lukuvi ametoa kauli hiyo Jijini Dodoma alipokuwa akizungumza na Wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika Mtaa wa Ndachi Kata ya Mnadani jijini Dodoma wakati
akikagua nyumba ambazo zimejengwa bila kufata utaratibu na kukosa vibali vya ujenzi.
Waziri Lukuvi alifikia hatua ya kusimamisha ujenzi kwa kuziwekea alama nyumba ambazo ujenzi wake umekiukwa na kuwaamuru wamiliki kusitisha shughuri zote hadi wafuate utaratibu.
Hata hivyo Mhe. Lukuvi amesema Serikali haina mpango wa kubomoa nyumba za wananchi isipokuwa wananchi wanatakiwa kujenga kwa kufuata utaratibu ikiwa ni pamoja na kupata kibali cha ujenzi.

No comments :

Post a Comment