Friday, January 31, 2020

DKT. POSSI AWATAKA WATUMISHI WA WIZARA YA HABARI KUFANYA KAZI KWA UADILIFU.



Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt.Ally Possi akizungumza na wafanyakazi wa Wizara yake leo Jijini Dodoma wakati alipokua akifunga Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ambalo amewakumbusha watumishi hao kufanya kazi kwa uadilifu na weledi mkubwa kwa maendelo ya Wizara na taifa kwa ujumla.
Mkurugenzi Idara ya Utawala na Rasilimali watu wa Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Bw.Bernad Patrick akiwasilisha mada kuhusu idara yake katika Baraza la wafanyakazi wa wizara hiyo lilifanyika kwa siku mbili januari 30 -31 Jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Bw.Petro Lyatuu akiwasilisha mada kuhusu Utekelezaji wa Bajeti ya mwaka 2019/2020 na vipaumbele vya bajeti ya 2020/2021 katika Baraza la wafanyakazi wa wizara hiyo lilifanyika kwa siku mbili januari 30 -31 Jijini Dodoma.
*****************************
Na Shamimu Nyaki – WHUSM, Dodoma.
Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Ally Possi amewataka watumishi wa Wizara hiyo kuendelea kufanya kazi kwa bidiii, uadilifu na kufuata sheria na kanuni za Utumishi wa Umma ambao ndio muongozo wa utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku katika kuwahudumia wananchi.

Dkt. Possi ameyasema hayo leo wakati wa kufunga kikao cha Baraza la Wafanyakazi lililofanyika kwa siku mbili Jijini Dodoma lililokua na lengo la kupokea taarifa ya utekelezaji wa bajeti kwa mwaka 2019/2020 na kuweka vipaumbele vya bajeti ijayo 2020/2021 pamoja na kujadili namna bora ya kusukuma mbele gurudumu la Wizara na kuboresha maslah ya wafanyakazi ili kuongeza tija na kuleta ufanisi katika utendaji wao wa kazi.

“Baraza hili limedhamiria kuleta mabadiliko katika Wizara yetu yatakayoleta matokeo chanya, natoa wito kwa wafanyakazi kuendelea kufanya kazi kwa uadilifu kujituma na kushirikiana ili Wizara yetu ilete maendeleo yaliyokusudiwa na nchi” alisema Dkt. Possi.

Aidha, amewataka Wakuu wa Idara kuondoa umbali uliopo kati yao na watumishi bali washirikiane na wawe wazi kujadili majukumu ya idara kwa upendo na pia waepushe upendeleo ili Wizara iwe sehemu nzuri ya kufanya kazi kwa uhuru.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa tawi la TUGHE Wizara ya Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo Bw. Mfaume Said amesema kuwa Baraza limekua na manufaa kwa kuwa hoja zilizowasilishwa na watumishi zimefafanuliwa vizuri na ambapo anaamini wafanyakazi watazifanyia kazi kwa weledi zaidi ili kuleta matokeo yanayokusudiwa.

No comments :

Post a Comment