Waziri wa Afya Hamad Rashid
Mohamed akizungumza na Muakilishi Mkaazi wa Shirika la Kuhudumia Watoto
UNICEF Maha Damaj alipofika Ofisini kwake Mnazi mmoja Zanzibar.
Waziri wa Afya Hamad Rashid
Mohamed akizungumza na Waandishi wa Habari baada ya mazungumzo yake na
Muakilishi Mkaazi wa Shirika la Kuhudumia Watoto UNICEF Maha Damaj
alipofika Ofisini kwake Mnazi mmoja Zanzibar.
*************************************
Na Ali Issa Maelezo Zanzibar 4/11/2019.
Waziri wa Afya
Zanzibar Hamad Rashidi Mohamed ameliomba Shirika la kuhudumia watoto
Duniani UNICEF kufanya utafiti juu ya hali ya utapiamlo kwa watoto ambao
wanakumbwa na
tatizo hapa nchini
Hayo ameyasema
leo huko Ofisini kwake wakati akizungumza na Mwakilishi mkazi wa
Shirika hilo kanda ya Zanzibar Maha Damaj, amesema Zanzibar imekuwa na
uzalishaji mkubwa wa chakula, matunda na mboga mboga lakini bado
kumekuwa na ongezeko la tatizo hilo nchini.
Amesema tatizo la
utapiamlo huwaathari watoto wengi kutokana na kukosa vyakula vyenye
afya ambalo limeonekana katika vituo vya afya na skuli.
Amesema ipo haja
ya kufanya utafiti ili kujua njia ya kuondosha tatizo hilo pamoja na
kuelimisha jamii juu ya madhara na kuwakinga watoto na madhara hayo.
“Watoto ndio
taifa la kesho hivyo ipo haja yakuona wanakuwa vizuri kwa kupata
vijana wenye afya na kulitumikia taifa lao badae”, alieleza Waziri
Hamad
Waziri Hamad
amesema maeneo yaliyoathirika zaidi na tatizo hilo ni Wilaya Micheweni
kwa upnde wa Pemba na Mkoa wa Kaskazini Unguja ni maeneo ambayo
yameonekana kutokea kwa vifo vingi vya kinamama na watoto.
Nae Mwakilishi
Mkazi Bi Maha Damaj Shirika lake litalishughulikia suala na kufanya
utafiti na kuhakikisha kwamba wanalipatia ufumbuzi na kujua sababu ya
tatizo hilo katika maeneo hayo.
Aidha amesema
kuwa yupo tayari kuitangaza Zanzibar na kuifanya kuwa ni kituo cha elimu
ya malaria kutokana na mafanikio makubwa ya kutokomeza maradhi hayo kwa
asilimia 0.2 jambo ambalo ni faraja kubwa duniani.
Hata hivyo
Muwakilishi huyo amesema kuwa shirika lake litatoa vifaa vya kina mama
na watoto katika vituo vya afya 36 vya Unguja na Pemba.
No comments :
Post a Comment