Meneja
miradi mwandamizi wa Taasisi ya WATER AID Tanzania, Bw.Twaha Mubarak
akizungumza na wanahabari katika ofisi za taasisi leo jijini Dar es
Salaam.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Mazingira
na Watu (UMAWA) inayofanya biashara ya usafi wa mazingira katika
upakuaj wa vyoo na uchakatishaji wa maji taka, Bw.Mathias Milinga
akizungumza na wanahabari katika ofisi za taasisi ya Water Aid leo
jijini Dar es Salaam.
*********************************
NA EMMANUEL MBATILO
Kuelekea siku ya Vyoo Duniani
wadau mbalimbali wa Afya nchini wametakiwa kutambua changamoto
zinazowakabili watu ambao wanajihusisha na uzibuaji wa mitalo mikubwa
pamoja na kutapisha mashimo ya Vyoo.
Katika jiji la Dar es Salaam pekee zaidi yq asimilia 70 ya wakazi wake yapo katika maeneo ambayo si rasmi.
Maeneo hayo sifa zake kunakuwa na
changamoto za upatikanaji wa maji safi na Salama, upatikanaji wa huduma
za usafi pamoja na huduma za utupaji wa taka maji.
Ameyasema hayo leo Meneja miradi
mwandamizi wa Taasisi ya WATER AID Tanzania, Bw.Twaha Mubarak katika
kikao cha waandishi wa habari kwenye ofisi za taasisi ya WATER AID
jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na wanahabari Bw.
Twaha amesema kuwa inakadiliwa asilimia 10 ya jiji la Dar es Salaam
limeunganishwa katika mfumo wa maji taka hivyo kunakuwa na uwezekano
mkubwa wa kuibuka magonjwa mbalimbali yanayoambukiza.
“Tukizungumzia katika asilimia
hizo, asilimia 90 zilizobaki tunatumia aina nyingine za mifumo, moja kwa
moja tunatakiwa kufahamu wanaofanya kazi hizo (kutapisha vyoo) ni wale
ambao wanaitwa majina mengi kama vyura ama wavamiaji lulu”. Amesema Bw.
Twaha.
Aidha Bw. Twaha amesema kuwa
katika ripoti ambayo imeandaliwa imezungumzia changamoto hizo kwa mfanya
usafi na imesheheni na kudadavua mkanganyiko wanaopitia wafanyakazi
katika sekta ya usafi kwenye nchi zinazoendelea.
Vilevile Bw.Twaha amesema kuwa
ripoti hii imeandikwa kwa pamoja kwa shirika la kazi Umimwwnguni,
Shirika la Water Aid, Benki kuu ya Dunia na Shirika la Afya Duniani,
lengo hasa ni kuinua ufahamu juu ya mazingira hatarishi ambayo
wafanyakazi hao wanayapitia.
Pamoja na hayo Bw. Twaha amesema
kuwa Wafanyakazi hao mara nyingi hugusa kinyesi cha binadamu pasipokuwa
na vifaa vya kujikinga wala vitendea kazi vilivyobora, kitu ambacho
kinawaweka kwenye hatari za kupata magonjwa mbalimbali.
Naye Mkurugenzi wa Taasisi ya
Mazingira na Watu (UMAWA) inayofanya biashara ya usafi wa mazingira
katika upakuaj wa vyoo na uchakatishaji wa maji taka, Bw.Mathias Milinga
amesema kuwa biashara hiyo imekuwa kwa kiasi tangu kuanzishwa kwake
kwani mpaka sasa katika maeneo mengi hasa wilayani Kigamboni upakuaji
holela wa vyoo umepungua kwa kiasi kikubwa.
“Wapakuaji wa kienyeji wakipata
kazi mara nyingi wanakuja kwenye kituo, tumefauru kupanua huduma hiyo
kwa kufanya matangazo katika vipeperushi lakini pia tunafanya kazi na
halmashauri hasa kamati za afya”. Amesema Bw.Milinga.
No comments :
Post a Comment