WAFANYAKAZI
wa Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) Kanda ya Dar es Salaam na Pwani
wakiongozwa na Meneja Mwandamizi wa Kanda hiyo, Mhandisi Hassan Said,
leo Agosti 16, 2019 wamefika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kitengo
cha Damu Salama na kuchangia damu ili kuwasaidia majeruhi wa ajali ya
moto wa gari la mafuta Morohgoro lakini na wale wenye uhitaji wa damu na
hawana jamaa wa kuwasaidia.
Utaratibu
wa wafanyakazi wa TANESCO kujitolea damu ni wakawaida ambapo mwkaa jana
walijitolea damu kwenye hospitali ya Tumbi Kibaha Mkoani Pwani.
Kanda
ya Dar es Salaam na Pwani inaundwa na Mikoa ya TANESCO Kinondoni
Kaskazini, kinondoni Kusini, Temeke, Ilala na Mkoa wa Pwani.
Meneja
Mwandamizi wa Kanda hiyo, Mhandisi Hassan Said, akijiandaa kwa zoezi
hilo kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam leo Agosti
16, 2019.
No comments :
Post a Comment