Makamu
Mwenyekiti wa Chama Cha Maafisa Habari wa Serikali (TAGCO), Bi. Sarah
Msika (kulia), akisalimiana na Meneja Mkuu wa TAZARA upande wa Tanzania
Bw. Fuad Abdallah (kushoto), huku Afisa Uhusiano wa TAZARA-Tanzania,
Bi.Regina Tarimo (katika) na mjumbe wa TAGCO,Bi.Gaudensia Simwanza
(wapili kulia), wakishuhudia wakati Bi. Msika alipokuwa akiwatembelea
maafisa habari wa Serikali kwenye mabanda mbalimbali ya taasisi
wanazofanyia kazi kwenye viwanja vya Nyakabindi Mkoani Simiyu kwenye
maonesho ya Nanenane kitaifa Mkoani Simiyu.
Afisa Uhusiano Mwandamizi wa Mfuko wa
Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Bw. Sebera Fulgence (kushoto), akifafanua
jambo kwa Makamu Mwenyekiti wa TAGCO Bi. Sarah Msika alipotembelea banda
la Mfuko huo viwanja vya Nanenane Mkoani Simiyu.
Afisa Uhusiano wa Tume
ya Nguvu za Atomiki Tanzania, (TAEC)Bi. Angela Msangi (kulia),
akizungumza na Bi. Msika kwenye banda la Tume hiyo viwanja vya Nanenane
Nyakabindi Mkoani Simiyu.
Meneja
Uhusiano wa TTCL, Bw. Nicodemus Mushi (kulia), akiwa ametembelewa na
Makamu Mwenyekiti wa TAGCO, Bi. Sara Msika (wapili kushoto) na mjumbe wa
Chama hicho, Bi. Gaudensia Simwanza kwenye banda la TTCL viwanja vya
Nakabindi kwenye maonesho ya Nanenane kitaifa Mkoani Simiyu.
NA
K-VIS BLOG/Khalfan Said, Simiyu
MAAFISA
habari wa Serikali wamepongezwa kwa kazi nzuri wakati wakitekeleza majukumu yao
katika kipindi cha maonesho ya Nanenane kitaifa kwenye viwanja vya Nyakabindi
Mkoani Simiyu.
Pongezi
hizo zimetolewa na Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Maafisa Habari wa Serikali
(TAGCO), Bi. Sarah Msika wakati alipokuwa akiwatembelea Maafisa hao kwenye
mabanda mbalimbali ya taasisi za Serikali zilizoshiriki maonesho hayo ambayo
yanafanyika kwa mara ya pili mfululizo kwenye viwanja hivyo.
“Kwanza
kabisa napenda niwapongeze maafisa habari wa Serikali ambao wako hapa kwenye
viwanja vya Nyakabindi Mkoani Simiyu kwenye maonesho ya Nanenane kwa
kuziwakilisha vema taasisi zao kwa kufafanua shughuli mbalimbali za Taasisi
hizo za Umma zinavyowahudumia wananchi.” Alisema Bi. Msika.
Pia
alisema amefurahishwa na mwamko wa maafisa habari hao wa Serikali ambao wengi
wamejiunga na TAGCO ambayo lengo lake ni kuwaleta pamoja Mafisa hao kwa lengo
la kubadilishana uzoefu katuka kuhakikisha taarifa za shughuli za serikali
zinawafikia wananchi kwa usahihi na kwa muda muafaka.
Maonesho
ya Nanenane yanafikia kilele Alhamisi Agosti 8, 2019 ambapo licha ya kufanyika
kitaifa Mkoani Simiyu, pia yalifanyika katika kanda tatu za Kaskazini ambapo
yalifanyika jijini Arusha, Kanda ya Mashariki yalifanyika Mkoani Morogoro na
Kanda ya Nyanda za Juu Kusini yalifanyika jijini Mbeya.
Kaulimbiu
ya mwaka huu ni “Kilimo, Ufugaji na Uvuvi kwa Ukuaji wa Uchumi wa Nchi.
No comments :
Post a Comment