Mkurugenzi
Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Waziri Kindamba amesema
mwaka huu wanatoa gawio la Sh2.1 bilioni kwa Serikali kutokana na kukua
kwa mapato ukilinganisha na mwaka uliopita.
Ameyasema hayo leo Jumanne ya Mei 21, 2019 katika hafla ya utoaji wa
gawio kwa Serikali iliyoenda sambamba na uzinduzi wa awamu ya pili ya
huduma ya video conference.
Kindamba amesema katika mwaka uliopita mapato yalikuwa Sh119 bilioni na mwaka huu imefikia Sh167 bilioni.
Akizungumza na wafanyakazi wa TTCL, Magufuli amesema: “Tangu Shirikia la
TTCL lianze kuendeshwa na wabia wetu, halikuwahi kutoa gawio hata la
shilingi tano kwa miaka 15 na lilikuwa likipata hasara ya Tsh bil.15 kwa
mwaka, lakini tangu tulirudishe kwenye mikono ya serikali, shirika hili
sasa limeanza kutengeneza faida kubwa.
“Niseme kwa uwazi, TTCL mmekuwa mkipigwa vita sana, vita zingine sio za
uwazi ni vita vya chinichini, hata leo kuja hapa kulikuwa na mbinu za
kijanja-kijanja kunizuia nisije kupokea gawio, na zimechezwa kwelikweli,
hii inathibitisha kuwa nyinyi mnastahili, lazima tuwasaidie.
“Waziri amesema Mfuko wa Mawasiliano upo chini ya wizara yake, pesa
zinachangwa na Watanzania na TTCL ni ya Watanzania, kwa nini inakodi
minara ya mashirika mengine na kulipia Sh mil. 700 hadi mil. 800? Kwa
nini usitumie pesa hizo kujenga minara ukawapa TTCL moja kwa moja?
“Mashirika mengine yanalipia kodi, lakini TTCL wanalipa kodi na wanalipa
gawio, kwa hiyo faida itayakopatikana itakuwa ni ya serikali, hakuna
haja ya kuwaacha TTCL wakateseka, huwezi kumuacha mwanao anateseka na
chakula unawapa watu wengine, lazima tuisaidie TTCL.
“Naomba niletewe orodha ya viongozi ambao wanatumia laini za TTCL na sio
ziwepo tu bila kutumika, huwezi kulipwa mshahara wa Serikali na hutumii
mtandao huo, asije akawa anaandika meseji tu halafu anaicha, nataka
ziwe zinatumika, sijamaanisha msitumie mitandao mingine. Msajili wa
Hazina hakikisha ifikapo mwezi Julai, mashirika yote 253 nchini ambayo
yamekuwa hayatoi gawio kwa serikali, yawe yametoa gawio la sivyo
yafungwe.
“Taasisi zilizojiunga kutumia TTCL, ofisi yangu ya rais haikutajwa,
chama changu CCM hakikutajwa, inaonekana hawa hata kwenye ofisi yangu
wamo. Kama wananisikia ninataka ndani ya mwezi mmoja tuanze kutumia simu
za TTCL na wizara nyingine,” amesema.
No comments :
Post a Comment