Wednesday, April 24, 2019

TBL YAZIDI KUMWAGA KOMPYUTA MASHULENI,SAFARI HII MWANZA


Mwanza donation media 1
Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Dk Severine Lalika(kushoto) akipokea moja ya kompyuta 10 kutoka kwa Meneja wa Kiwanda cha bia cha TBL Mwanza Patel Kilovele, zilizotolewa na kiwanda hicho kwa ajili ya shule za msingi na sekondari za kata ya Pasiansi jijini Mwanza, na printa tatu kwa ajili ya kituo cha kulelea watoto wanaoishi katika mazingira magumu cha KKKT Misungwi.kulia ni Meneja Raslimali Watu wa TBL Mwanza,Dora Nyambalya.
Mwanza Donation media 3
Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Dk Severine Lalika (kushoto) akipokea moja ya printa tatu kwa ajili ya kituo cha kulelea watoto wanaoishi katika mazingira magumu cha KKKT Misungwi na  kompyuta 10  kwa ajili ya shule za msingi na sekondari za kata ya Pasiansi jijini Mwanza,zilizotolewa na kampuni ya bia ya TBL.
COMPUTER MWANZA 1
Walimu wakuu na Wakuu wa Shule za Sekondari na Msingi wa kata ya Pasiansi, wakijaza fomu ya kupokea Kompyuta 10 kutoka kampuni ya TBL kwa ajili ya shule zao, kwenye hafla iliyofanyika jijini Mwanza.
COMPUTER MWANZA 2
Meneja wa kiwanda cha TBL Mwanza Patel Kilovele  akiongea wakati wa hafla  hiyo (kulia) ni Meneja Rasilimali watu wa kiwanda hicho Dora Nyambalya.
 ………………………
Kampuni ya Tanzania Breweries Limited (TBL),baada ya kutoa msaada wa kompyuta mpakato 20  kwa shule 3 tatu za sekondari mkoani Dar es Salaam,wiki hii imetoa msaada wa kompyuta 10 na
printer 3 kwa ajili ya shule za msingi na sekondari za kata ya Pasiansi jijini Mwanza, na printa tatu kwa ajili ya kituo cha kulelea watoto wanaoishi katika mazingira magumu cha KKKT Misungwi.
Akiongea wakati wa kukabidhi msaada huo,Meneja wa kiwanda cha TBL cha Mwanza,Patel Kilovele,alisema msaada huo ni mwendelezo wa kampuni kusaidia huduma za kijamii katika maeneo ambayo inafanyia biashara zake sambamba na kuunga mkono jitihada za serikali kukabiliana na changamoto mbalimbali.
“TBL tutaendelea kusaidia kukabiliana na changamoto mbalimbali za kijamii , kwa kuwa hivi sasa tuko katika ulimwengu wa kidigitali tumeona ni vema shule zetu nazo zipate kompyuta kwa ajili ya kurahisisha kazi na kuboresha elimu,”alisema Kilovele

No comments :

Post a Comment