Saturday, November 10, 2018

Tambua haki yako kama mwanachama wa mfuko wa hifadhi ya jamii (1)

HakiPensheniBuilding relationship with in laws

Na Christian Gaya

www.majira.co,tz Ijumaa 09 November 2018

Haki ya taarifa kwa mwanachama kwa wakati huu wa mabadiliko ni ya muhimu sana, ukichukulia asili ya ugumu wa mifuko ya pensheni ya hifadhi ya jamii na juu ya ugumu wa uelewa wa elimu ya fedha na pensheni kwa wanachama na kwa wananchi kwa ujumla.
Kama miaka kadhaa tumetoka kwenye mfumo rahisi wa hifadhi ya jamii wa kuweka akiba ambapo hali hatarishi zote za mfuko wa akiba huachiwa mwanachama pekee na kuingia ...
kwenye mfumo mgumu zaidi wa mpango wa pensheni ya hifadhi ya jamii unaondeshwa kwa mfumo wa bima ambapo mwanachama anaahidiwa mafao yote kwa mkataba maalumu atakayopatiwa kuanzia mwanzo anapojiunga yakiwepo ya muda mfupi na ya muda mrefu.
Mwanachama kupata taarifa na kummilikisha kwa njia ya kumhamisisha na kumwezesha awe uwezo wa kufanya maamuzi. Mara nyingi mwanachama anapatiwa habari na kujua kinachoendelea inakuwa ni magurudumu mazuri zaidi ya kuongeza mwendo wa uwazi na uwajibikaji wa uongozi wa mifuko ya pensheni ya hifadhi ya jamii.
Ikumbukwe ya kuwa mifuko ya pensheni huudwa chini ya bodi ya wadhamini wanaokuwa na wajibu wa kusimamia wanaosimamia mfuko. Haki ya kupata habari kwa upande mmoja ina maana ni haki ya wanachama kujua mfuko wao wa pensheni na kwa upande mwingine ni wajibu wa bodi ya wadhamini kutoa habari kwa wanachama wa mfuko
Kila mfuko unasimamiwa kablasha ya sheria linaloeleza wazi taratibu, vigezo na masharti ya mfuko. Katiba hii kumbukumbu ya habari na taarifa zote zinazohusu mfuko. Ni jambo la muhimu ya kuhakikisha ya kuwa mwanachama wanajizoesha wenyewe na sheria za mfuko wao na hata kuziweka na kuziandika kwenye vijitabu vidogo ambayo vimefupisha habari  zote za msingi zinazohusu mfuko.
Kijitabu kidogo kinalenga kuwa na maelezo yote muhimu kwa lugha ya wazi na rahisi kusomeka bila kwenda nje ya katiba ya mfuko. Bila ya kuzingatia mfuko uko mazingira gani inapotoa mpango wa pensheni kwa wanachama, haki ya kupata habari ziko katika njia nne zifuatazo.
Taarifa za Msingi za Mfuko
Wanachama wanatakiwa wawe na uwezo wa kujibu maswali ya msingi yanayohusu mfuko wao, kama vile: ni akina nani wadhamini wa mfuko? Ni nani anastahili kuwa mwanachama wa mfuko? Ni jinsi gani wanachama wanaunda mafao? Je wanachama wanachangia kwenye mfuko? Ni kiasi gani wanachama wanachangia? Je mwajiri anachangia? Ni kiasi gani mwajiri anachangia? Ni umri wa miaka mingapi wanachama wanatakiwa kustaafu kwa hiyari au mapema Ni baada ya miaka mingapi wanachama wanastahili kustaafu kwa lazima? Ni mafao ya gani wanachama wa nastahili kupata kabla na baada ya kustaafu kazini?
Taarifa hizi zote zinaweza kupatikana kwenye katiba, kajitabu cha mwanachama (kama kipo) au kwa kuuliza idara ya mawasiliano, masoko na huduma kwa wateja au ofisi yeyote zilizotapakaa karibu nchi nzima
Makablasha ya Kisheria.
Pamoja na katiba ya sheria, wanachama wana haki ya kukagua mahesabu ya mfuko yaliyokaguliwa kisheria na mkaguzi mkuu wa mahesabu ya serikali. Mwanachama vile vile ana haki ya kukagua nyaraka kama vile marejista yote yanayoyotunza kumbukumbu za mfuko pamoja na taarifa za uwekezaji
Kumbuka ya kuwa, mfuko umeanzishwa kwa ajili ya kumnufaisha mwanachama wake na kazi kubwa ya wadhamini ni kulinda maslahi ya mwanachama kwenye mfuko
Mkutano mkuu wa Mwaka wa Wanadau na Wanachama
Mifuko yote inatakiwa kufanya mkutano mkuu wa wanachama na wadau ambapo wanachama wanaalikwa kuhudhuria. Wanachama wanaohudhuria wanapata taarifa zote na matukio mbalimbali kutoka kwa wadhamini wa mfuko na kwa watoa huduma ambao ni viongozi wa mfuko, wakaguzi wa mahesabu, wataalamu na mameneja wa mfuko pamoja na wawakilishi wa umoja wa vyama vya wafanyakazi makazini, na wawakilishi wa serikali. Mkutano mkuu unatoa fursa kwa wanachama kuuliza maswali kwa wadhamini na watoa huduma juu ya kila kitu kinachohusu mfuko.
Pamoja na kupata matukio yote yanayohusu utendaji na maendeleo ya mfuko, mkutano mkuu hutoa nafasi kwa wanachama juu ya mabadiliko yoyote yanayohusu mafao ndani ya mfuko na jinsi mafao yao yatakavyoleta mabadiliko yeyote. Kwa kweli badiliko lolote juu ya mafao yanatolewa na mfuko lazima yataambatana na mabadiliko ya sheria na vigezo pamoja na masharti yake.
Taarifa za Mahesabu ya wanachama
Wanachama wanastahili kupewa taarifa zao kila mwisho wa mwaka wa fedha. Hizi taarifa za hutoa taarifa juu ya mafao mwanachama anayostahili kila mwisho wa mwaka unaofanyiwa mabadiliko
Kwa mwanachama wa mfuko wa akiba ya wafanyakazi, taarifa hutoa maelezo juu ya michango iliyochangiwa na mwanachama na mwajiri wake, na riba iliyopitishwa na wadhamini kwa mwisho wa mwaka na idadi ya michango yote ya mwanachama pamoja na riba ya mwisho wa mwaka. Na kwa wanachama wa mfuko wa pensheni unaondeshwa kwa mfumo wa bima.
Mfuko wa pensheni unaoshughulika na wafanyakazi wa sekta binafsi yaani NSSF, na mfuko wa pensheni wa kwa ajili ya watumishi wa umma (PSSSF) hupewa maelezo juu ya aina za mafao ambayo mwanachama anastahili kupatiwa na mfuko kama vile mafao ya muda mrefu na ya muda mfupi ambapo yote huendeshwa kwa mfumo wa bima.
Haki ya kupatiwa taarifa inahamasisha uwazi, ufahamu na uelewa na uwajibikaji wa mifuko ya hifadhi ya jamii. Pia inamwandaa mwanacham kupata fursa ya kuhakikisha na kulinganisha taarifa ili kulinganisha na kufananisha na ukweli na michango yao  Pamoja na kuwa na haki ya kupata taarifa, wanachama pia lazima wajue juu ya haki za mafao na haki zao zingine kwa ujumla.
Taarifa za Mahesabu ya wanachama
Wanachama wanastahili kupewa taarifa zao kila mwisho wa mwaka wa fedha. Hizi taarifa za hutoa taarifa juu ya mafao mwanachama anayostahili kila mwisho wa mwaka unaofanyiwa mabadiliko
Kwa mwanachama wa mfuko wa akiba ya wafanyakazi, taarifa hutoa maelezo juu ya michango iliyochangiwa na mwanachama na mwajiri wake, na riba iliyopitishwa na wadhamini kwa mwisho wa mwaka na idadi ya michango yote ya mwanachama pamoja na riba ya mwisho wa mwaka. Na kwa wanachama wa mfuko wa pensheni unaondeshwa kwa mfumo wa bima
Mfuko wa pensheni unaoshughulika na wafanyakazi wa sekta binafsi yaani NSSF, na mfuko wa pensheni wa kwa ajili ya watumishi wa umma (PSSSF) hupewa maelezo juu ya aina za mafao ambayo mwanachama anastahili kupatiwa na mfuko kama vile mafao ya muda mrefu na ya muda mfupi ambapo yote huendeshwa kwa mfumo wa bima.
(Inaendelea wiki ijayo)




No comments :

Post a Comment