MKURUGENZI
Mkaazi wa Shirika la Savings Bank Foundation for International
Cooperation Steven Noel Safe akizungumza kwenye hafla ya kufunguliwa
kwa ofisi za shirika hilo lisilo la kiserikali katika eneo la Bwiru ,
Ilemela jijini Mwanza.kushoto kwake ni Mtendaji Mkuu wa Benki ya Akiba
ya Tubingen Ujerumani Dr. Christoph Gogler ambaye alikuwa mgeni rasmi.
Wa kwanza kushoto ni Meneja miradi wa SBFIC Mwanza, Tom.
Mtendaji
Mkuu wa Banki ya Akiba ya Tubingen Ujerumani Dr. Christoph Gogler
akiangalia machapisho yanayotumika kutoa elimu ya kuweka akiba kwa
wanafunzi wa shule za sekondari na msingi huku Mkurugenzi Mkaazi wa
SBFIC Steven Noel Safe akimpa maelezo kuhusiana na machapisho hayo.Kulia
wa kwanza ni Mtendaji Mkuu wa taasisi ya Self Micro Finance Fund,Mudith
Cheyo.Shirika hilo linajenga miradi endelevu na kutoa elimu na kutafuta
ufumbuzi bora wa masuala ya kifedha kwenye taasisi na vyama vya kuweka
na kukopa.
Mtendaji
Mkuu wa Benki ya Akiba ya Tubingen Ujerumani Dr. Christoph Gogler
akikata utepe kufungua ofisi huku Mkurugenzi Mkaazi wa SBFIC Steven
Noel Safe , mwenye kinasa sauti akishuhudia (kulia wa kwanza).
Mtendaji
Mkuu wa Benki ya Akiba ya Tubingen Ujerumani Dr. Christoph Gogler
ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa ofisi za SBFIC jijini
Mwanza akikata keki.Wa kwanza kulia anayeshuhudia ni Meneja miradi wa
SBFIC Mwanza, Steven Noel Safe.
Mtendaji Mkuu wa Benki ya Akiba
ya Tubingen Ujerumani Dr. Christoph Gogler ambaye alikuwa mgeni rasmi
kwenye ufunguzi wa ofisi za SBFIC jijini Mwanza akilishwa keki na Leah
Michael, mwanafunzi wa kidato cha tatu katika Shule ya Sekondari
Karagwe.Wa kwanza kulia anayeshuhudia ni Meneja miradi wa SBFIC Mwanza,
Steven Noel Safe.
Picha zote na Baltazar Mashaka
………………………
NA BALTAZAR MASHAKA, MWANZA
SHIRIKA
la Savings Bank Foundation for International Cooperation (SBFIC) liko
kwenye mikakati ya kutoa elimu (mafunzo) ya fedha kwa taasisi ndogo
ndogo za kifedha nchini ili
kutafuta ufumbuzi bora wa masuala ya kuweka
na kukopa fedha.
Pia
shirika hilo lisilo la kiserikali linalenga kujenga uhusiano wa muda
mrefu utakaoliwezesha kushirikiana na taasisi hizo kukuza biashara na
kujenga miradi yao itakayokuwa endelevu hata baada ya wafadhili kuondoka
.
Mkurugenzi
Mkaazi wa SBFIC nchini, Steven Noel Safe akizungumza na waandishi wa
habari jana kwenye hafla ya ufunguzi wa ofisi za shirika hilo lisilo la
kiserikali,alisema wana mkakati wa kuwafundisha walimu wa walimu
watakaotoa elimu kwa wananchi hasa wajasiriamali namna ya kuweka na
kukopa kwenye taasisi za fedha.
Alisema
mkakati utakaoanza mwakani unawalenga walimu wa masuala ya elimu ya
fedha hasa wa shule kwa ajili ya wanafunzi, maofisa ushirika kwa ajili
ya vyama vya kuweka na kukopa na maofisa maendeleo ya jamii
watakaoelimisha vikundi vya kijamii vinavyokopa kwenye halmashauri.
Safe
alieleza kuwa wanataka kuwafikia wananchi wengi hivyo elimu hiyo ya
kuweka na kukopa itatolewa na watalaamu waliobobea kwenye masuala ya
fedha kutoka Ujerumani na nchi zingine kwa taasisi ndogo ndogo za MFIs
,Vicoba,Saccos, wakulima na wajasiriamali ili kutafuta ufumbuzi bora wa
kifedha na familia kuweza kupanga bajeti ya familia.
“Changamoto
kubwa ni Watanzania tunapopata miradi tusifikirie itadumu
milele,tunatakiwa tuifanye kwa weledi ili tuendelee.Pia tumezoea wageni
wanaotoa posho na hatutaki kuchangia chochote na wakiondoka miradi mingi
inakufa na hakuna maendeleo yoyote.Kwa elimu tunayotoa tunataka
mwananchi ajue kila kitu ili achague mwenyewe akakope wapi kwa riba
nafuu,”alisema Safe.
Mkurugenzi
huyo Mkaazi wa SBFIC alieleza kuwa kukiwa na ufanisi na ubora katika
taasisi ndogo ndogo za fedha kutachangia kukuza maendeleo ya kiuchumi ya
nchi, kwa kuwa uchumi mkubwa hujenga ajira na kukuza elimu ambayo ni
muhimu kwa Tanzania ya viwanda ili kufikia uchumi wa kati.
“Tumeanza
kufundisha wanafunzi wa shule za sekondari na msingi namna ya uwekaji
fedha na kuhusisha jamii nzima kwa kuwajengea uelewa wa masuala ya
Financial Inclusion (fedha).Tumezisaidia taasisi washirika wetu juu ya
masuala na mipango endelevu ya miradi yao, mikakati na utawala bora na
mafunzo katika kuendesha miradi hiyo baada ya kupata misaada wajiendeshe
wenyewe,maana kuna muda miradi itakoma, ”alisema.
Safe
akielezea mikakati ya kimenejimenti ya kukuza biashara ya taasisi
husika hadi sasa wamefanya kazi na Benki ya Posta (TPB), Karagwe
Development and Conservation Agency (KARUDECA),Tanzania Association of
Micro Finance Institutions (TAMFI),SELF Microfinance Fund na Tume ya
Ushirika Tanzania.
“Taasisi
hizo zimenufaika kwa kupata ujuzi na utalaamu wa fedha, weledi katika
utendaji kazi zao, kuboresha familia maskini na kuanzisha miradi
endelevu.Pamoja na kufanya kazi na taasisi hizo lengo kuu ni kuona namna
gani tutawafikia wananchi wengi zaidi,”alisema Mkurugenzi huyo Mkaazi
wa SBFIC.
Hata
hivyo alieleza zaidi kuwa mazungumzo baina ya serikali na SBFCI
yanaendelea ili kuona jinsi gani watafanya mafunzo hayo na yakiwa tayari
wataanzisha kufundisha elimu kwa vitendo hususani taasisi ndogo ndogo
za kifedha.
Akifungua
ofisi za SBFIC Mtendaji Mkuu wa Benki ya Akiba ya Tubingen ya
Ujerumani, Dr. Christoph Gogler alisema watatoa elimu kwa taasisi za
kifedha nchini na kujenga uwezo wa wananchi kutokana na kubobea kwenye
masuala ya fedha na kutumia utaalamu wao wa miaka 150.
Alieleza kuwa mbali na kufungua
ofisi amekuja kuangalia miradi inayofanyika Tanzania hasa katika eneo la
kifedha lengo likiwa ni kutoa elimu kwa wananchi juu ya kutunza akiba
ambapo pia kuitaziwezesha taasisi za fedha na benki humu nchini kupiga
hatua ya maendeleo na kujenga uchumi imara
No comments :
Post a Comment