Wednesday, September 19, 2018

SERIKALI KUWAINUA VIJANA KUPITIA KILIMO CHA MBOGA MBOGA KWA KUTUMIA KITALU NYUMBA(GREENHOUSE)


 Serikali inakamilisha zoezi la uhakiki wa maeneo yaliyotengwa na mikoa kwa ajili ya shughuli za vijana ili kutekeleza mpango wa kuwawezesha vijana vitalu nyumba na mafunzo ya kutengeneza vitalu nyumba.Mpango huu utaifikia mikoa 7 katika hatua ya mwanzo na baadaye kuifikia mikoa mingi zaidi hasa kutokana na utayari wa mikoa husika katika kutenga maeneo ya kilimo kwa Vijana.
Hayo yamesemwa Septemba 18, 2018 mkoani Simiyu na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi,Vijana na Ajira Mhe. Anthony Mavunde (pichani anayemwagilia) wakati akikagua maeneo yaliyotengwa kwa kilimo cha Vijana katika kijiji cha Mwamanyili-Wilaya ya Busega,Nyakabindi-Wilaya ya Bariadi na Kijiji cha Ngh’eshi-Wilaya ya Itilima,ambapo ameeleza dhamira ya Serikali ya kuwawezesha vijana katika kilimo ili kupunguza changamoto za Ajira kwa Vijana.
Naibu Waziri Mavunde pia amelipongeza Shirika la World Vision kwa kushirikiana na Mbunge wa Itilima Mh Daud Silanga Njalu kwa ujenzi wa kituo cha Maarifa ambacho kinawapatia Vijana mafunzo ya fani mbalimbali za Ufundi.
Wakati huo huo Mh Mavunde,amewataka uongozi wa Wilaya ya Halmashauri ya Itilima kuwapa zabuni ya kufyatua matofali ya ujenzi wa zahanati kwa vikundi vya Vijana kama njia ya kuviwezesha kufikia mafanikio yao ya kiuchumi.



No comments :

Post a Comment