Video: Zitto, Polepole watunishiana misuli mtandaoni, ‘Mzee wa kurukia treni kwa mbele ushaanza’
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi
(CCM), Humphrey Polepole na Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe
wameibua mvutano mkali katika mtandao wa kijamii wa ‘Twitter’.
Mvutano huo ni kufuatia mabadiliko madogo ya baraza
la mawaziri yaliyofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Dkt. John Pombe Magufuli.
Moja ya sababu kuu ni baada ya Zitto
kumpa pole Mwigulu baada ya kuachwa kando katika baraza la mawaziri na
kueleza kuwa aliponzwa na msimamo wake kuhusu Kanisa la Kiinjili la
Kilutheri Tanzania (KKKT).
Katika
mabadiliko hayo yaliyofanywa na Rais John Magufuli, Mwigulu Nchemba
ambaye alikuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi ameachwa.
Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Zitto aliandika kuwa;
“Ndugu yangu Mwigulu Nchemba karibu back bencha ufanye kazi ya
wananchi. Tunajua msimamo wako kuhusu barua ya KKKT (Kanisa la Kiinjili
la Kilutheri Tanzania) umekuponza, ulikuwa na msimamo madhubuti na
ulisimamia haki.”Hapo hapo mara tu baada ya ujumbe huo, Polepole
aliibuka na kumjibu, Zitto Kabwe ni mzee wa kurukia treni kwa mbele.
“Mzee wa kurukia treni kwa mbele ushaanza, mbona unapenda ubashiri na
vitendo vya kilozi. Rais hutenda impendezavyo kwa dhamana aliyopewa na
Katiba. Sisi tuliohudumu kwenye Serikali na chama tunajua na kuheshimu, usijitatafutie huruma kwa mtu acha kupotosha hiyo si siasa safi.”
No comments :
Post a Comment