Tuesday, July 24, 2018

KATIBU MKUU WA CCM, BASHIRU ALI APOKELEWA KWA KISHINDO MKOANI SINGIDA


 Kijana wa Chipukizi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Ikungi, Amina Abdallah akimvika skafu Katibu Mkuu wa CCM, Dk.Bashiru Ali baada ya kuwasili Wilaya ya Ikungi katika ziara ya kikazi ya siku moja mkoani Singida leo hii. Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Ikungi, Mika Tano Likapakapa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida, Hassan Kilimba.
 Kikundi cha Utamaduni cha Liti kikitoa burudani wakati wa mapokezi ya Katibu Mkuu, Dk.Bashiru Ali.
 Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida, Hassan Kilimba (kulia), akimuelekeza jambo Katibu Mkuu wa CCM, Bashiru Ali baada ya kuwasili wilayani Ikungi.
 Dk.Bashiri akisalimiana na viongozi mbalimbali baada ya kuwasili wilayani Ikungi.
 Dk. Bashiru akiwasalimia wana CCM.
  Dk. Bashiru akisaini katika kitabu cha wageni.
 Makada wa CCM wakiwa kwenye mkutano wa kupokea Katibu Mkuu.
 Mkutano ukiendelea.
 Wimbo wa Taifa ukiimbwa.
 Makada wa CCM wakiimba wimbo wa Taifa.
 Makada wa CCM wakijitambulisha kwa Katibu Mkuu.
 Katibu Mkuu wa CCM Mstaafu Mzee Yusuph Makamba akisalimiana na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Singida, Diana Chilolo.
  Katibu Mkuu wa CCM Mstaafu Mzee Yusuf Makamba akisalimiana na Katibu Mkuu wa CCM, Dk.Bashiru Ali. Katikati ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida, Hassan Kilimba.
Mbunge wa Singida Magharibi, Elibariki Kingu, akitoa taarifa ya utekelezaji wa shughuli za maendeleo katika Jimbo hilo, mbele ya Katibu Mkuu.

 Katibu Mkuu wa CCM Mstaafu Mzee Yusuph Makamba , akizungumza kwenye mkutano wa kumpokea Katibu Mkuu mkoani Singida.
 Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, .Miraji Jumanne Mtaturu, akitoa taarifa ya maendeleo kwa Katibu Mkuu.
 Katibu Mkuu wa CCM, Dk.Bashiru Ali akipitia taarifa mbalimbali za maendeleo.
 Kaimu Katibu wa CCM Wilaya ya Ikungi, Mussa Sunja, akitoa taarifa.
 Katibu Mkuu wa CCM, Dk.Bashiru Ali na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida, Hassan Kilimba wakionesha silaha za jadi baada ya Wazee wa Mkoa wa Singida kumsimika rasmi.

NAIBU Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso kulia akizungumza na Mhandisi wa Maji Korogwe Mji Joseph Mcharo kabla ya kumsimamisha kazi kulia ni Kaimu Mkuu wa wilaya ya Korogwe Godwin Gondwe
 NAIBU Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso kushoto akizungumza na watendaji wa Halmshauri ya Korogwe Mji wakati wa ziara yake
NAIBU Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso kulia akimsikiliza kwa umakini Kaimu Mkuu wa wilaya ya Korogwe Godwin Gondwe wakati wa ziara yake
NAIBU Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso amemsimamisha Mhandisi wa Maji Halmashauri ya Wilaya Korogwe Mji Joseph Mcharo kwa kutumia force accout kwenye mradi wa zaidi ya Milioni 700 bila ya kibali toka Wizara hiyo.
Agizo la kusimamishwa kwa Mhandisi huyo alilitoa jana wakati akikagua mradi miwili ya maji ya Mtonga ambao umetumia zaidi ya milioni 700 na msambiazi ambao umetumia zaidi ya milioni 600 ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya mkoa wa Tanga ambayo ilianza juzi wilayani Handeni.
Alisema mradi huo ulitakiwa kutumia kiasi cha shilingi Milioni 500 na wataalamu hao wakaubadilisha na kuufanya uwe wa milioni 700 ingawa bado unaendelea kusuasua jambo ambalo linaonyesha ubadhirifu wa fedha za Serikali
Akiwa kwenye mradi wa Mtonga baada ya kumalizika kuukagua alitilia mashaka na ndipo alipoamuru mhandisi huyo kumpatia maelezo ya kina kuhusiana na mradi huo lakini pia hakuridhika na maelezo hayo na kuagiza kuwa atapeleka wataalamu kutoka wizara ili kuweza kuhakiki thamani ya fedha na ubora mrai huo.
“Kwa kweli mimi hapa sijaridhika na utekelezaji wa mradi huu unaonekana upo chini ya kiwango na ucheleweshwaji huku wananchi wakiendelea kupata tabu hivyo nitatuma wataalamu kutoka wizarani waje kuhakiki mradi huo”Alisema
Baada ya ukaguzi wa mradi huo Naibu Waziri huyo aliambatana na viongozi mbalimbali wa halmashauri ya Korogwe mji kuelekea kwenye mradi wa Msambiazi ambako kunajengwa tenki kubwa la mradi utakaosambaza maji kwa wananchi.
Akiwa huku ndipo alipomuuliza mhandisi gharama za mradi ambapo alisema zaidi ya milioni 600 zimetumika kwa kutumia mfumo wa mkandarasi na kupelekea mradi huo kufikia kwenye hatua za mwisho jambo ambalo limeibua maswali mengi kwa Naibu Waziri na kuamua kuchukua uamuzi huo.
“Ndugu zangu haiwezekani mradi wa zaidi ya milioni 700 kutumia force account kinyume na taratibu za wizara huku mradi wa milioni 600 ukitekelezwa kupitia mkandarasi ni wazi kwamba kuna ubadhirifu unaendelea hapa na mimi sitakubali”Alisema.
Baada ya maelezo hayo Naibu Waziri aliamua kumsimamisha mkandarasi huyo kwa kigezo miradi inayotumia chini ya milioni 200 ndio inapaswa kutumia force acounti tofauti na alivyofanya mhandisi huyo huku akimdanganya kwamba anakibali kutoka wizarani.
Awali akijib u hoja za Naibu Waziri huyo Mhandisi wa Maji Halmashauri ya Korogwe Mji Joseph Mcharo alidai anakibali cha wizara kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa mtonga kutumia force acounti ndipo Naibu Waziri huyo alipoamua kupiga simu wizara kupata ufafanuzi.
Naye kwa upande wake Mkurugenzi wa Halamshauri ya Korogwe Mji Jumanne Shauri alionekana kushindwa kujibu maswali ya Naibu Waziri jambo ambalo liliibuka mabishoni baina yao kabla ya Kaimu Mkuu wa wilaya ya Korogwe Godwin Gondwe kumtaka Mkurugenzi akiri mapungufu yaliyojitokeza kwenye mradi huo.
Mradi wa Mtonga ambao Naibu Waziri Aweso aliitulia mashaka ni wa kusambaza tenki,mabomba na sehemu maalumu kwa ajili ya mtambo wa kutibia na kusafisha maji eneo la mradi husika

No comments :

Post a Comment