Aidha uhakiki huo unatarajiwa kufanyika kwa baadhi ya viongozi na si viongozi wote Nsekela amesema ni kutokana na Serikali kutokuwa na fedha za kutosha za kuhakiki viongozi wengi kwa wakati mmoja.
“Sasa tumefikia mahali ambapo tuende kuhakiki kwa baadhi ya viongozi nasema kwa baadhi ya viongozi kwasababu kuna sababu nyingi, sababu kubwa tunasema ni rasilimali fedha tunasema kwamba kama fedha hatuna za kutosha hatuwezi kuwahakiki viongozi wengi kwa hivi sasa tumefanya uchambuzi wa viongozi 900 ambao sasa tunakwenda kuwahakiki” Amesema Nsekela.
-
Kesi ya Mbowe na wenzake yagonga mwamba, wataka rufaa
-
Serikali kuchakachua sheria ya Uzazi na Afya, wanaume nao watajwa kunufaika
“Kama mnavyojua sisi tunazungumzia suala zima la maadili kwamba kiongozi awe na maadili na mimi kama kiongozi na mmoja wapo wa viongozi nikitoa tamko langu na nikitaka kuhakiki tunataka tujue zile mali nilizo nazo na uwezo wangu kuna uwiano gani hapo, hizo mali nimepata kihalali au sijapata kihalali” Amesema Nsekela
Aidha Disemba 27, 2017 Nsekela aliwahimiza Viongozi wa Umma kukamilisha taratibu za ujazaji wa fomu za tamko la rasilimali na madeni kabla ya Disemba 31 mwaka huo.
No comments :
Post a Comment