Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Elias Kwandikwa(kushoto) akisikiliza maelezo jana ya Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS) Mkoa wa Tabora, Mhandisi Damian Ndabalinze (wa
pili kutoka kulia) mara baada ya kukagua kipande cha barabara Tabora
hadi Nyahua kwa ajili ya kujionea wizi wa alama za barabarani na eneo
lililokarabatiwa la Nyahua kutokana na uharibifu uliosababishwa na maji
ya mvua ya kukata mawasiliano baina ya Itiga na Tabora.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Elias Kwandikwa( wa pili kushoto) alichungulia
jana mkondo wa maji katika eneo la Nyahua yaliyosababisha kipande
barabara katika eneo la Nyahua wilayani Uyui kukatika na kusababisha
mawasilano baina ya Tabora ya Itigi kukatika. Kushoto ni Meneja wa
Wakala wa Barabara (TANROADS) Mkoa wa Tabora, Mhandisi Damian Ndabalinze .
Naibu
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Elias Kwandikwa(kushoto)
akitoa maelekezo jana katika eneo la Nyahua wilayani Uyui kwa
Mwakilishi wa Kampuni ya CHICO Peng Hao (kulia) mara baada ya
kutembelea eneo la barabara ya Itigi hadi Tabora lililoharibiwa na maji
ya mvua.
Picha na Tiganya Vincent
………………..
NA TIGANYA VINCENT
RS TABORA
SERIKALI
imetangaza kutoa zawadi nomo kwa wananchi watakaosaidia kutoa taarifa
za siri za kuwafichua watu wanaong’oa alama za barabarani na
kuisababishia hasara kutokana na urejeshaji wake.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
Elias Kwandikwa mara baada ya kukagua
ukarabati wa eneo Nyahua ambalo lilikuwa limekatika kutokana na maji ya
mvua yaliyopelekea kukosekana kwa mawasiliano baina ya Itigi na Tabora
jana wilayani Uyui.
Alisema
Serikali imekuwa ikitumia fedha nyingi kuweka alama za barabara ili
kuwaongoza watumiaji wa barabara kuepuka ajali lakini baadhi ya watu
wamekuwa wakihuju na kung’oa alama hizo kwa ajili ya kwenda kuziua kama
vyuma chakavu.
Kwandikwa
alisema mtu atakayesaidia kutoa siri ya wanaong’oa alama hizo na
wanunuzi wake atapewa zawadi na jina lake halitafichuliwa kwa ajili ya
usalama wake.
Alisema
inasikitisha kuona kuwa alama zipatazo 78 zenye thamani ya shilingi
milioni 27 katika kipande cha barabara ya urefu kilometa zipatazo 80.6
kutoka Tabora hadi Nyahua zimeng’olewa.
Naibu
Waziri huyo alisema alama hizo zinatumia fedha nyingi za Serikali kwa
kuwa baadhi yake zinatoka nje ya nchi na kuongeza kuwa vitendo hivyo ni
hatari sana ni vema wahusika wakikamatwa washitakiwe kama wahujumu
uchumi.
Alisema
hata pale Serikali ilipoamua kujengwa alama hizo kwa Sementi bado
baadhi ya watu wamekuwa wakizivunja ili kutoa nondo zilitumika katika
ujenzi wake.
“Fikiria
katika muda wa siku moja alama zaidi ya moja alama za barabarani 30
mkoani Kilimanjaro zimeng’olewa … Je? Kwa mwezi ni alama ngapi
zinang’olewa ..pesa ngapi za Serikali inapotea kurudisha alama hizo …Ma
RC na Ma DC na wananchi saidieni katika kupambana na wahujumu wa
miundombinu katika maeneo yenu” alisema Kwandikwa.
Aidha
Naibu Waziri huyo alisema hatua kali zitachukuliwa dhidi ya wauzaji na
wanunuzi wa vyuma chakavu watakoa patikana na alama za barabara ili iwe
fundisho kwa watu wanohujumu miundimbinu.
Kwandikwa
alisema jamii inawajua vema wanaonunua vyuma chakavu ni vema wakatoa
taarifa za siri ili kukomesha tatizo hilo ambalo limekuwa likichangia
sehemu ya ajali nyingine za barabarani.
“Meneja wa TANROADS nafikiri
tuanze kutoa kiasi fulani cha fedha kwa mtu anayetusaidia kutoa taarifa
za siri kwa watu wanaong’oa alama za barabarani ili tukomesha tatizo”
alisema Naibu Waziri.
Hivi karibuni Kamati ya Kudumu
ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikiwa katika ziara yake ya
kikazi Mkoani Tabora ilielezea kusikitishwa kwake na wizi wa alama za
barabarani katika barabara nyingi za Mkoa huo na kuagiza viongozi wa
maeneo husika ambapo barabara kuu zinapita wasimamie ulinzi.
No comments :
Post a Comment