Friday, March 2, 2018

FINCA MICROFINANCE YATIMIZA MIAKA 20 KWA MAFANIKIO NCHINI TANZANIA



1
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya FINCA Microfinance, Tanzania Issa Ngwegwe akizungumzia mafanikio ya sherehe zake FINCA Microfinance kutimiza miaka 20 ya utendaji wake wa shughuli za kifedha nchini Tanzania tangu kuanzishwa kwake.
2
Mwenyekiti wa Bodi ya FINCA ambaye pia ni Makam wa Rais na Mkurugenzi wa Kanda ya Afrika Mike Gama-Lobo akizungumza katika mkutano huo.
3
Rais na Mkurugenzi Mtendaji wa FINCA Microfinance Holding Company, Andree Simon akiipingeza FINCA Microfinance kwa kufanya kazi kwa ufanisi wa hali ya juu.
…………………………………………………………………………………..
Banki ya FINCA Microfinance, miongozi mwa benki maarufu zinazotoa mikopo midogo midogo nchini Tanzania, kwa mafanikio makubwa wakati ikiwa imefikisha miaka 20 tangu kuanzishwa kwake hapa Tanzania.
Issa Ngwegwe amesema hayo katika mkutano na waandishi wa habari kwenye hoteli ya Serena jijini Dar es salaam wakati akiwaeleza waandishi wa habari kuhusu sherehe za taasisi hiyo   na Mafanikio  ya miaka 20 ya FINCA katika kutoa huduma za kifedha zilizo salama na
kuwezesha wajasiriamali wadogo nchini Tanzania  ambapo mgeni rasmi katika hafla hiyo anatarajiwa kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mheshimiwa Samia Sululu Hassan
Amesema  sherehe hizo zinatarajiwa kuhudhuriwa na zaidi ya wageni 300 ambao ni Bodi ya Wakurugenzi wa FINCA, Uongozi wa FINCA, wafanyakazi na viongozi wa juu kutoka katika mtandao wa FINCA pamoja na wageni waalikwa mbalimbali.
Akielezea kuhusu  hali ya ukopeshaji ya FINCA, Ngwegwe amesema: “Tangu FINCA ilipoanzishwa mwaka 1998, imeweza kutoa zaidi ya shilingi za Kitanzania  900 Billioni katika mikopo kwa wateja zaidi ya milioni 1.1  wakiwemo wajasiriamali wadogo, kukuza biashara zao,  kutengeneza ajira na kuboresha kiwango cha maisha yao”.
Katika miaka ijayo FINCA itaendelea kutekeleza wajibu wake katika kuboresha upatikanaji wa huduma za kifedha kwa wafanyabiashara wadogo (SMEs) ambao ndio msingi wa maendeleo ya uchumi wa nchi yetu hasa vijijini. 
Ameongeza kuwa FINCA  imejidhatiti katika mpango wake wa kuondoa umasikini kupitia suluhisho la kudumu ambalo linasaidia watu kujenga rasilimali zao, kutengeneza ajira na kuboresha kiwango chao cha maisha kiuchumi.
Kwa upande wa Rais na Mkurugenzi Mtendaji wa FINCA Microfinance Holding Company, Andree Simon aliipongeza FINCA Tanzania kwa safari yake yenye mafanikio ambayo imewafikisha katika miaka 20 ya maendeleo na mabadiliko, yaliyosaidia taasisi hiyo kuendelea kuwa taasisi ya kutoa mikopo midogo na kufikia kuwa Benki ya kutoa mikopo midogo kama ilivyo sasa.
Mwenyekiti wa Bodi ya FINCA ambaye pia ni Makamu wa Rais na Mkurugenzi wa Kanda ya Afrika Mike Gama-Lobo aliwashukuru wajumbe wenzake wa Bodi na viongozi wa juu wa Benki kwa kuonyesha juhudi za kuigwa ambazo zimepelekea katika kukua kwa FINCA, kufikia maendeleo makubwa katika mazingira ya biashara yenye changamoto nyingi.

No comments :

Post a Comment