Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiingia kwa gari maalum akiwa na Mkuu
wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Venance Mabeyo wakati wa maadhimisho ya
miaka 56 ya Uhuru wa Tanzania yaliyofanyika kwenye uwanja wa Jamhuri
mjini Dodoma ambako ndiyo makao makuu ya Nchi. maadhimisho hayo
yamehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali ,Mabalozi wa
wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini, viongozi wa vyama vya siasa,
Viongozi wa dini pamoja na wananchi wa viunga vya mji wa Dodoma, Mh.
Rais Dkt. John Pombe Magufuli pia amemsamehe Nguza Viking “Babu Seya” na
Mwanaye Johnson Nguza “Papii Kocha” waliokuwa wamefungwa Kifungo cha
Maisha Gerezani.(PICHA NA JOHN BUKUKU-FULLSHANGWE-DODOMA)
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikagua gwaride huku akiongozwa na
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Venance Mabeyo wakati wa maadhimisho
ya miaka 56 ya Uhuru wa Tanzania yaliyofanyika kwenye uwanja wa Jamhuri
mjini Dodoma
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akielekea jukwaa kuu mara baada ya
kukagua gwaride huku akiongozwa na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali
Venance Mabeyo wakati wa maadhimisho ya miaka 56 ya Uhuru wa Tanzania
yaliyofanyika kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mh.Jenista Mhagama Waziri Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu baada ya kukagua gwaride katika maadhimisho ya miaka 56 ya Uhuru wa Tanzania yaliyofanyika kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma
Picha mbalimbali zikionyesha
Vikosi vya Ulinzi vikitoa heshima kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli
Amiri jeshi mkuu wa majeshi ya Uinzi wakati wa maadhimisho ya miaka 56
ya uhuru kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma leo.
Kikosi cha Makomandoo wa Jeshi la Ulinzi JWTZ kikipita kwa Gwaride la heshima mbele ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli.
Baadhi ya wananchi mbalimbali waliohudhuria katika maadhimisho hayo wakiwa jukwaa kuu.
Makomandoo wakionyesha onyesho lao la kuokoa kiongozi aliyetekwa kwa kushuka na Helkopta ya kijeshi.
No comments :
Post a Comment