Rais wa Chama Cha PRST, Loth Makuza akizungumza jambo.
Meza kuu ilivyoonekana.
Msaidizi wa Mkurugenzi wa Idara ya
Habari( MAELEZO), Jonas Kamaleki akipokea cheti cha Rais Mstaafu wa
Awamu ya Tatu Benjamin Mkapa, kutokana na mchango wake wa kuagiza idara
za serikali kuwa na msemaji.
Baadhi ya wageni waalikwa waliohudhuria hafla hiyo.
Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya, Suzan Mbise aliyekuwa mmoja wa wageni waalikwa akizungumza jambo.
Wakiwa katika picha ya pamoja.
CHAMA Cha Maofisa Uhusiano wa Umma
(PRST) kimezinduliwa jijini Dar es Salaam, ambapo maudhui makubwa ya
kuundwa kwa umoja huo ni kutambulika rasmi kama taasisi na kupanuana
mawazo ya utumishi miongoni mwa wanachama, ikiwa ni pamaoja na kuendesha
shughuli zao kwa utaratibu maalum.
Akihutubia katika uzinduzi huo,
mgeni rasmi ambaye ni Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na
Michezo, Ndege Makula aliwasisitizia wanachama juu ya kudumisha maadili
ya umma katika utumishi wao huku akitilia mkazo suala la kujali misingi
ya taaluma na matakwa ya sheria katika kulitumikia taifa.
“Nawaomba mtambue kuwa kupitia
ummoja wenu huu ninyi mmebeba dhamana kubwa ya kuhakikisha mnatumika
ipasavyo kwa wananchi, kwa hiyo cha muhimu ni kuzingatia maadili na
misingi ya taaluma yenu ikiwa ni pamoja na kufuata sheria inataka nini,
vinginevyo niwatakieni utumishi mwema katika nafasi hizi muhimu kwa
jamii,” alisema Makula.






No comments :
Post a Comment