Friday, November 24, 2017

Wahitimu Chuo Cha Maendeleo Tengeru Watakiwa Kutafsiri Elimu Yao Kwa Vitendo


A
Mgeni rasmi katika Mahafali ya Chuo  cha Maendeleo ya Jamii Tengeru ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Arusha Bw. Gabriel Fabiani akikabidhi zawadi kwa mwanafunzi bora wa shahada ya kwanza Maendeleo ya Jamii Usimamizi wa program za maendeleo ya jaimii Bi.Fotunata Kaniki.
B
Wajumbe wa bodi ya Chuo  cha Maendeleo ya Jamii Tengeru wakiwa katika picha ya pamoja na badhi ya wahitimu leo Tengeru Jijini Arusha.
C
Kaimu Mkuu wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii Tengeru Dr. George Bakari akiwahutubia wahitimu mbalimbali wa Chuo hicho leo Tengeru  jijini Arusha .
D
Mgeni rasmi katika Mahafali ya Chuo  cha Maendeleo ya Jamii Tengeru ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Arusha Bw. Gabriel Fabiani akitoa hotuba yake kwa wahitimu mbalimbli hawapo pichani leo katika chuo hicho Tengeru nje kidogo ya jiji la Arusha.
E
Mgeni rasmi katika Mahafali ya Chuo  cha Maendeleo ya Jamii Tengeru ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Arusha Bw. Gabriel Fabiani akitoa hotuba yake kwa wahitimu mbalimbli hawapo pichani leo katika chuo hicho Tengeru nje kidogo ya jiji la Arusha.
………..
Mgeni rasmi katika Mahafali ya Taasisi  ya Maendeleo ya Jamii  Tengeru amewataka wahitimu mbalimbali Katika chuo hicho kutafsiri elimu waliyoipata kwa vitendo akiwataka kutanguliza maslahi ya Jamii badala ya maslahi binafsi ambayo ...
yamelitafuna Taifa kwa kipindi kirefu sasa.
Aidha mgeni rasmi hiyo bwana Gabriel Fabian ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Arusha amesema wasomi wamelitia Taifa hasara kwa kusaini mikataba mibovu na kupokea rushwa akiwataka wahitimu hao kutumia elimu kwa manufaa ya wale walioikosa na Taifa kwa ujumla.
Aidha amewataka wahitimu hao kuangalia fursa nyingine nje ya taaluma yao na kuacha tabia yakutaka ajila za mfumo rasmi ambazo zina ushindani mkubwa kwa kuwa taaluma Kama ya kwao inatolewa na taasisi nyingine za elimu ya Juu .
Mkuu huyo wa Wilaya pia amesisitiza matumizi sahihi ya Maktaba akisema kuwa waihitimu wengi siku hizi wanatumia makaburasha na vitini vya wahitimu wa zamani badala ya kusoma vitabu ambavyo uandikwa na wanazuoni wakubwa duniani.
Wakati huohuo Makamu Mkuu wa Taasisi ya Chuo cha Maendeleo ya Jamii Tengeru Dk.George Bakari amesema
Kwasasa chuo chake kipo katika mageuzi makubwa ya kuhakikisha chuo hicho kinakua kitaaluma kwa kujenga mahusiano makubwa na taasisi nyingine za kitaaluma ndani na nje ya nchi ikiwemo kubadilishana wahadhili na kujenga uwezo wa kitafiti .
Dr. Bakari ameongeza kuwa Chuo chake kwa sasa kinaendelea pia kuchukua hatua anwai za kuendeleza watumishi wanataaluma na wasio wanataaluma kielimu ili waweze kujiimarisha kielimu ili kuendana na mabadiliko yaliyopo  sasa katika wigo mpana wa sayansi na teknolojia.
Chuo hiki chini ya Mwanazuoni huyo pia kinaratibu uanzishwaji wa bodi ya taaluma ya kada ya maendeleo ya Jamii hapa nchini ambapo ametumia fursa hiyo ya Mahafali kuwataka wahitimu kujiunga mara moja na umoja wa wanataaluma wa maendeleo ya Jamii.
Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Tengeru imewatunuku wahitimu wake astashahada,shahada,na stashahada ya kwanza ya maendeleo ya Jamii mwaka wa masomo 2016/17

No comments :

Post a Comment