Mkurugenzi
Mkuu wa PSPF, Adam Mayingu, akimkabidhi Baturi Msusi kadi yake ya uanachama wa
PSPF itakayomwezesha hata kupata fursa ya kupewa mkopo wa kuanzia maisha mpango
unaojulikana kama jipanga kimaisha na PSPF.
Na CHRISTIAN GAYA
Idadi kubwa ya waajiriwa
wapya hutumia mapato yao yanayotokana na malipo ya mishahara ya mwisho wa mwezi
kuimarisha kujipanga kimaisha ambapo mishahara hiyo haitoshi kuwawezesha kumudu
gharama kama kulipa kodi ya nyumba au kununua samani.
Waajiriwa wapya hasa wakiwa
ni vijana wamekuwa wakipata ugumu wa kupata kipato cha kuanzia maisha ili
kujipanga vizuri kimaisha. Karibu idadi kubwa ya wafanyakazi hapa nchini wote
wamepitia hali hii na kukumbuka walivyoanza kazi na kuhitajika kwa mahitaji
kadhaa, lakini walikwamishwa na kipato.
Mishahara
ya waajiriwa wapya tu mara nyingi haiwezi kukidhi mahitaji yao ya lazima
kimaisha kama vile kununua samani za ndani, kulipa kodi ya nyumba, kununua
chombo cha usafiri, kugharamia vyombo vya ndoa na harusi. Matokeo yake
waajiriwa wapya wengi wameishi kwa kuunga unga tu bila ya kuwa na vyanzo vya
fedha vyenye uhakika na hivyo bila kukidhi matakwa yao mapya ya ajira.
Kwa
kutambua hili PSPF wameanzisha huduma ya mkopo wa wanachama wapya unaomwezesha
mwanachama mpya mchangiaji wa PSPF kujipanga kimaisha.
Mkurugenzi
Mkuu wa PSPF, Adam Mayingu anasema mpango wa mkopo wa kuanzia maisha wa
mfuko wa PSPF unaojulikana kama “Jipange Kimaisha" mkopo kwa mwajiriwa mpya
umelenga kumwezesha kumudu gharama za mahitaji muhimu ili kukidhi matakwa
halisi ya maisha ya waajiriwa wapya ambao ni mwanachama wachangiaji wa mfuko wa
PSPF.
Lengo
kubwa la mfuko wa PSPF kuanzisha mkopo huu wa kuanzia maisha ni kuhakikisha ya
kuwa kila mtanzania anatimiza ndoto yake kwa kupitia mkopo wa kuanzia maisha. Kabla
ya mpango huu wa mkopo wa kuanzia maisha, waajiriwa wapya walikuwa hawana fursa
ya kupewa mikopo kutokana na taasisi za fedha kuwa na hofu ya usalama wa mikopo
yenyewe .
"Hivi
ndivyo PSPF ilivyojipanga kwa kuanzisha huduma ya mkopo wa wanachama wapya
unaomwezesha mwanachama mpya kujipanga kimaisha kwa kumudu gharama za maisha na
kuwa msaada mkubwa sana kwa vijana wengine wakaoingia katika ajira,"
mkurugenzi mkuu anasema.
Anasema
waajiriwa wapya wengi wameanza kunufaika na huduma hii, na wameanza kupeleka taarifa
kwa waajiriwa wapya, hasa walioko vijijini na nje ya nchi ambao taarifa za aina
hii kwao hawajazipata kwa wakati unaotakiwa na kuhakikisha ya kuwa mpango huu
wa mkopo wa kuanzia maisha unawanufaisha idadi kubwa ya wanachama wapya wa PSPF
nchini.
"Madhumuni ya kuanzisha mpango huu wa jipange kimaisha
na PSPF ni kuwajali wanachama wetu hata wakiwa katika mwanzo wao wa ajira na
hiyo inakwenda sambamba na kaulimbiu yetu ya PSPF tulizo la wastaafu" Mayingu
anasema.
Anasema mwajiriwa mpya ambaye atajisajiri kuwa mwanachama
mchangiaji wa PSPF atastahili kupata mkopo huu wa kujipanga kimaisha baada ya
kuchangia kwenye mfuko wa PSPF kwa kipindi cha miezi isiyopungua sita.
"Mwanachama huyo mpya atakayejiunga na PSPF anaweza
kukopa hadi kufikia mishahara ya miezi miwili; mfano: kama mwanachama mshahara
wake kwa mwezi ni shilingi milioni 1,000,000/ ina maana anaweza kupata mkopo wa
kuanzia maisha wa shilingi milioni 2,000,000 za kitanzania kwa mkupuo na huku
akilipa taratibu,"anafafanua zaidi.
Anaeleza ya kwamba huduma
ya kuanzia maisha ni huduma muhimu sana kwa vijana kwani upataji wa fedha za
kujiendeleza kwa kundi hili imekuwa changamoto kubwa hivyo kupatikana kwake imeanza
kufungua milango kwa vijana
kujimudu gharama za kulipa kodi ya nyumba, kununua samani za ndani, kugharamia
ndoa na harusi, kununua chombo cha usafiri n.k. bila vikwazo.
Hivyo
natoa wito kwa watanzania wenzetu kujiunga na mfuko wa pensheni wa PSPF ili
waweze kufaidika na fursa hii,” Mayingu anasisitiza.
Mwandishi wa makala hii ni mwanzilishi wa
Kituo cha HakiPensheni, mshauri na mtaalamu wa masuala ya pensheni. Kwa maelezo
zaidi gayagmc@yahoo.com unaweza kutembelea
tovuti hakipensheni
monitor online na hakipensheni blog +255 655 13 13 41
No comments :
Post a Comment