Tuesday, November 28, 2017

GEPF na michango ya pensheni ya umilikishwaji nyumba mwanachama



Mkurugenzi Mkuu wa GEPF Daud Msangi, sheria  ya mfuko inatamka wazi ya kuwa mwanachama anaweza kutumia sehemu ya mafao yake kama dhamana ya kupata mkopo wa nyumba ya makazi.

Na CHRITIAN GAYA

Kutokana na upeo wa michango au mafao ya pensheni, umilikaji wa nyumba ni sehemu ya upangaji mzuri wa jinsi ya kustaafu. Kumiliki nyumba wakati wa kustaafu inawalinda wastaafu kutokana na mahitaji ya mtiririko wa fedha mkononi. Pamoja na hayo tena inawalinda ...
wastaafu kutokana na maamuzi mabaya ya uwekezaji, na faida mbaya inayotokana na uwekezaji ikiwemo na mfumuko wa bei ambao hauendi na ukali wa maisha wa wakati huo.

Nyumba inamwandaa mstaafu na maisha yenye heshima usoni mwa jamii na yenye utu mzuri wa hali ya maisha. Umilikaji wa nyumbani kwa kweli huchangia kiasi kikubwa kwa wastaafu kwa ajili ya kuwaandaa maisha ya ulimwengu wa kustaafu na katika kuwatengenezea staili ya miaka yao ya mwanzoni kabla hawajastaafu.

Singapore wanachama wa mfuko wa hifadhi ya jamii wanaruhusiwa kutumia asilimia 75 ya akiba yao ya michango ya pensheni kwa ajili kukopeshewa nyumba au kwa ajili ya kununulia nyumba maalumu anayohitaji.

Nyumba ni rasilimali ambayo inawezekana kubadilishana na kitu chochote. Kwa sababu thamani ya nyumba inatambulika. Kijamii nyumba inachangia kuhamasisha na kuboresha nafsi ya mtu, utu, usalama na kutambuliwa mbele za watu. Kisiasa, nyumba bora inapunguza vitishia vya kisiasa vinavyotokana na kugandamizwa na kuchanganyikiwa hasa kwa watu wanaoishi kwa mazingira hatarishi na makazi yasiyokuwa rasmi

Wakati Mauritius na Afrika Kusini mifuko ya hifadhi za jamii yanaruhusu kutoa mikopo moja kwa moja kwa wanachama na hata vilevile wanachama kutumia sehemu ya theruthi mbili ya mafao yao ya baadaye kama amana ya kumpatia mikopo benki na kupata mkopo wa nyumba kutoka taasisi za nyumba au mashirika ya nyumba ya nchi hizo kama vile Shirika la Nyumba la Taifa.

Mafao yaliyosalia yanaachwa kama yalivyo bila kuguswa mpaka wanachama atakapofikia wakati wa kustaafu kwa hiari au kwa lazima. Wanachama waliokopa wanalipa riba kwa muda wote na kuhurusiwa kuingilia mafao kulipa deni halisi alilokopa wakati utakapofika muda wake wa kawaida wa kustaafu. Kwa Afrika kusini viongozi wa hifadhi ya jamii wanapandisha mkopo wa nyumba kwa kutumia soko la mtaji kwa kutoa amana ya pensheni ili kumwezesha mwanachama kumiliki nyumba

Katika kutambua umuhimu wa ungezeko wa uzalishaji nyumba kwa ajili ya kuhudumia watu wanaongezeka kila siku, mkurugenzi mkuu wa GEPF, Daud Msangi anasema serikali mara kwa mara  imekuwa ikiaangalia uwezekano wa kuwa na ufumbuzi  wa aina mbalimbali na hata vilevile kushawishi ushiriki wa sekta za watu binafsi ili kufikia lengo hili la nyumba. Uwezekano wa kupata mikopo ya fedha kwa waendelezaji na wanunuzi kumekuwa ni mojawapo ya sababu zilizochangia kuwa na uhaba wa nyumba.

Anasema Sheria ya Mfuko wa mafao ya kustaafu GEPF ya mwaka 2013 inayoanzishwa kwa manufaa ya waajiriwa katika sekta rasmi na isiyo rasmi ikijumuisha watu waliojiari wenyewe,  inatoa amana ya mkopo wa nyumba ya makazi katika kutambua umuhimu wa jambo hili kwa wastaafu wake.

"Inatamka wazi ya kuwa mwanachama wa Mfuko wa GEPF anaweza kutumia sehemu ya mafao yake kama dhamana ya kupata mkopo wa nyumba ya makazi kulingana na utaratibu ulioelekezwa na mamlaka. Na kuonesha ya kuwa sheria hiyo inakwenda na wakati hasa kwa kuwajali wateja wake inasema wazi ya kuwa mwanachama anaweza kwa ruhusa ya bodi kuchukua sehemu ya michango yake kwa namna na kwa kiasi kitakachokuwa kimeainishwa kwenye Kanuni," Msangi anafafanua zaidi.

Anasema kulingana na Sheria ya GEPF ya mwaka 2013 amana ya mwanachama” maana yake ni michango ya mwajiriwa, michango ya mwajiri na riba yake ambayo ipo kwenye akaunti ya mwanachama. Sheria hiyo inaruhusu wanachama wake kuingilia michango yao ya akiba ya pensheni kwa ajili ya amana ya kujipatia nyumba ya mkopo. 
 
"Mkopo huu ni kwa ajili ya kujenga nyumba ya mwanachama wa GEPF na hutolewa kwa mwanachama aliyefikisha umri wa miaka 55 ambaye amechangia kwa muda usiopungua miezi 180," Msangi anakumbusha zaidi. 

Mwandishi wa makala hii ni mwanzilishi wa Kituo cha HakiPensheni, mshauri na mtaalamu wa masuala ya pensheni. Kwa maelezo zaidi gayagmc@yahoo.com unaweza kutembelea tovuti hakipensheni monitor online na hakipensheni blog Simu  +255 655 13 13 41

No comments :

Post a Comment