Kupitia
tuzo hizo zinazotambulika kama PAHA, kituo cha Televisheni cha Clouds
kimetambuliwa kama kituo bora cha Runinga kwa mwaka 2017.
Hiyo
ni kutokana na kurusha maudhui yanayomulika maisha ya watu na kutoa
tumaini kwao kupitia vipindi na kampeni mbalimbali kama vile…
(#IshiNaMimi #Kipepeo #MalkiaWaNguvu #RudishaTabasamuMiaMoyo na nyinginezo)
Baada
ya kupokea tuzo hiyo ya heshima Kampuni ya Clouds Media Group
imeishukuru YUNA pamoja na umoja na umoja wa mataifa kutokana na
Utambuzi huo.
Sambamba na hilo Clouds Tv imewashukuru Watanzania Kwa kuendelea Kuwaamini na Kuwachagua.
”
Tunaahidi kuendelea kuwatumikia kwa moyo na nguvu zaidi kwani
tulishakula kiapo cha kuwa Taasisi ya watu” sehemu ya taarifa hiyo
ilieleza.
(#RedioYaWatu #ThePeoplesStation)
#TunakufunguliaDuniaKuwaUnachotaka
No comments :
Post a Comment