Baadhi ya wanunuzi wa korosho wakiwa wanasubiri uzinduzi wa mnada wa kwanza wa korosho mkoani Pwani ,uliofanyika wilayani Kibiti
Mkuu wa Mkoa wa Pwani mhandisi
Evarist Ndikilo wa kwanza kulia akitoka kuangalia ghala la korosho huku
akiwa ameambatana na Mkuu wa wilaya ya Kibiti, Gulamhussein Kifu siku ya
uzinduzi wa mnada wa kwanza wa korosho Mkoani hapo uliofanyika Kibiti
Picha na Mwamvua Mwinyi
……………
Na Mwamvua Mwinyi,Kibiti
MNADA wa kwanza wa ununuzi wa
korosho ,mkoani Pwani uliofanyika wilayani Kibiti ,umefanikiwa kuuza
korosho daraja ya kwanza kwa bei ya sh. 3,817 kwa kilo huku daraja la
pili ikinunuliwa kwa sh .2,950.
Bei hiyo imeongeza katika msimu
huu tofauti na msimu ...
wa mwaka 2015/2016 ambapo korosho daraja la kwanza
ilinunuliwa kwa sh.2,900 kwa kilo na daraja la pili sh.2,500.
Licha ya mnada huo kufanikiwa
lakini mkoa huo bado unahitaji magunia 200,000 kwa ajili ya kuhifadhia
korosho zilizovunwa msimu huu ambazo zinafikia zaidi ya tani 25,000.
Mkuu wa mkoa wa Pwani ,Mhandisi
Evarist Ndikilo akizindua mnada huo alieleza msimu huu mavuno yamekuwa
ni makubwa na korosho ni nyingi .
Alieleza kutokana na hilo magunia yanahitajika kwa wingi ili kuhifadhi korosho hizo.
Mhandisi Ndikilo alisema kuwa
,walipatiwa magunia 30,000 ambayo hayakutosheleza kwani yote yameisha na
bado kuna mahitaji makubwa licha ya kwamba wamehakikishiwa hivi
karibuni yatapelekwa magunia mengine.
Alielezea wilaya ya Kibaha na
Kisarawe zilishindwa kufika kwenye mnada huo kutokana na kukosa magunia
ya kuhifadhia korosho na mkoa unafanya kila njia kuhakikisha magunia
hayo yanapatikana.
“Changamoto hii inabidi
tukabiliane nayo kwa kukaa na mikoa ya Lindi na Mtwara ili kuhamasisha
wawekezaji waje wawekeze kiwanda cha magunia lengo likiwa ni kukabiliana
na tatizo hili,” alisema mhandisi Ndikilo.
Nae mkuu wa wilaya ya Kibiti
Gulamhussein Kifu alisema ,wakati wanahifadhi korosho ambazo
zimenunuliwa wataingia mikataba na vyama vya msingi ambavyo ndiyo wenye
korosho ili kusitokee kupungua kwa korosho zilizohifadhiwa.
Alibainisha kumekuwa na changamoto
ya kupungua kwa korosho ambazo zimehifadhiwa hivyo kusababisha
malalamiko kwa wanunuzi na kwa watakaohusika watachukuliwa hatua za
kisheria.
Ofisa Kilimo wa Wilaya ya Kibiti,
Bainga Bwenda alisema, kwenye mnada wa kwanza wamepata kilo milioni 3.8
za daraja la kwanza imezidi minada sita ya mwaka jana kwa kilogramu
100,000.
Anasema kuna mafanikio makubwa
yaliyotokana na serikali kutoa pembejeo bure na mfumo wa stakabadhi
ghalani lakini changamoto iliyojitojeza ni uhaba wa magunia .
No comments :
Post a Comment