Monday, October 23, 2017

TBL Group yaadhimisha mwezi wa Saratani ya Matiti Duniani kwa vitendo

KANA KONYAGI 5
Dk.Fatma Kiango kutoka hospitali ya wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam akitoa mada kuhusiana na ugonjwa wa Saratani ya matiti kwa baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya TDL.
KANSA MBEYA 6
Dk.  Joseph Matemba kutoka Shirika lisilokuwa la kiserikali la JHPIEGO- Mbeya akitoa  mada ya Saratani ya matiti kwa wafanyakazi wa kiwanda cha TBL-Mbeya
KANSA MWANZA 4
Dk. Fridolin Mujuni kutoka hospitali ya Bugando jijini Mwanza akitoa mada kuhusiana na ugonjwa wa Saratani ya matiti kwa baadhi ya wafanyakazi wa kiwanda cha TBL cha Mwanza.
SARATANI DAR 1
Baadhi ya wafanyakazi wa kiwanda cha TBL cha Ilala wakimsikiliza  Dk.Namwai Makame alipokuwa akiwapatia maelezo kuhusiana na Saratani ya matiti wakati wa zoezi la kuwapima wafanyakazi wa kampuni hiyo lililofanyika kiwandani hapo.
………………………………………………………………
-Yaendesha zoezi la kupima afya za wafanyakazi
 
Wafanyakazi wa kampuni ya  TBL Group katika viwanda vyote nchini mwishoni mwa wiki walipimwa Saratani ya matiti ikiwemo kupatiwa elimu juu ya ugonjwa huu ambao umekuwa ukiongezeka kwa kasi nchini.
Meneja Mawasiliano wa Mawasiliano wa  kampuni hiyo,Zena Tenga,amesema kuwa zoezi hili limetekelezwa nchini ya Mpango wa kuimarisha afya za... wafanyakazi pamoja na familia zao unaojulikana kama ‘Afya Kwanza’ ikiwa pia ni kuadhimisha mwezi wa Saratani ya matiti duniani  kwa vitendo.
Tenga amesema  tangu mpango huu uanze kutekelezwa na kampuni umeanza kuonyesha mafanikio makubwa kwa kuwa wafanyakazi wanapata fursa ya  kupata elimu ya afya ya kujikinga na magonjwa mbalimbali  elimu ambayo pia inatolewa wa familia za wafanyakazi.
“Mwitikio wa wafanyakazi wetu wote kushiriki katika programu hii ni mzuri kama ambavyo wengi wamejitokeza kupimwa na kupatiwa ushauri wa jinsi ya kuepuka ugonjwa wa Saratani ya Matiti na kujua dalili za ugonjwa huu mapema pindi unapojitokeza ili kuwahi kufanyiwa uchunguzi na kupata matibabu”.Alisema Tenga.
 
Alisema mbali na kampuni kuwa na utaratibu mzuri wa kuhakikisha wafanyakazi wake na familia zao wana bima ya afya na kuwa na zahanati katika viwanda vyake bado imeonelea kuna umuhimu wa kuhakikisha wanapata elimu ya kinga kwa kuwa kinga ni bora kuliko matibabu na kuongeza kuwa mbali na wafanyakazi kupatiwa elimu na ushauri nasaha kuhusiana na magonjwa mbalimbali pia wanapata fursa ya kushiriki kufanya mazoezi ya pamoja yanayoshirikisha pia familia zao pia wamekuwa wakipatiwa elimu kuhusiana na masuala ya umuhimu wa lishe bora.
“Changamoto ya ongezeko la magonjwa  nchini inachangiwa na sababu mbalimbali mojawapo ikiwa ni mitindo ya maisha ya kisasa na ukosefu wa elimu ya lishe bora,kupitia jukwaa hili  la Afya kwanza wengi wanaelimika na kujua umuhimu wa mazoezi,lishe bora na mtu mwenye afya njema anatakiwa awe katika hali gani”.Alisema Tenga.
 
Tenga alisema katika kufanikisha zoezi hili  la kupima Saratani ya Matiti kampuni imetumia wataalamu wa afya kutoka hospitali mbali kama ambavyo imekuwa ikifanya katika utekelezaji wa Programu ya Afya Kwanza.
Mmoja wa madaktari walioendesha zoezi la kupima Saratani kwa wafanyakazi na familia zao jijini Dar es alaam,Dk.Fatma Kiango kutoka hospitali ya wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam,amesema kuwa Tanzania ni moja ya nchi ambazo zimekuwa na ongezeko kubwa la wagonjwa wa saratani kwa kasi hususani katika miaka ya karibuni mojawapo ikiwa ni saratani ya Matiti ambayo inaendelea kuathiri wanawake wengi.
 
Alibainisha baadhi ya sababu za ugonjwa wa  saratani ya matiti kuwa  ni historia ya  saratani katika  familia, mfumo wa kazi unaoweza kusababisha kansa ,mfumo wa maisha kama vile uvutaji wa sigara, mfumo wa kula. “Ni muhimu kutafuta matibabu ya haraka, ukiona dalili zozote za saratani ya matiti, usisubiri mpaka uwe katika hali mbaya ndio uende hospitali, kwa sababu baada ya kuchunguzwa mapema  unaweza kutibiwa kwa ufanisi,” alisema Dk. Kiango.

No comments :

Post a Comment