Thursday, August 31, 2017

DKT PALLANGYO AKUTANA NA KAMPUNI YA M & P EXPLORATION PRODUCTION TANZANIA LIMITED


PICHA NA 1
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (kulia) akiongoza kikao kilichoshirikisha watendaji kutoka Kampuni inayojihusisha na utafiti na uchimbaji wa gesi ya M & P Exploration Production Tanzania Limited, Wizara ya Nishati na Madini, Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO)  na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC)
PICHA NA 2
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (kulia) akizungumza na Meneja Mkuu kutoka Kampuni inayojihusisha na utafiti na uchimbaji wa gesi ya M & P Exploration Production Tanzania Limited, Christophe Maitre ( kushoto) katika kikao hicho.
PICHA NA 3
Sehemu ya watendaji kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO)  na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) wakifuatilia maelekezo yaliyokuwa yanatolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (hayupo pichani) katika kikao hicho
…………………..
Leo Agosti 31, 2017 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo amekutana na Kampuni inayojihusisha na utafiti na uchimbaji wa gesi ya M & P Exploration Production Tanzania Limited kwenye Ofisi za Wizara ya Nishati na Madini zilizopo jijini Dar es Salaam lengo likiwa ni kujadili namna ya kuendeleza gesi ya Mnazi Bay. Kikao hicho pia kilishirikisha watendaji kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO)  na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC)

No comments :

Post a Comment