Wednesday, July 12, 2017

Wabunge kutoka Uganda watembelea taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete

KC1
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Profesa. Mohamed Janabi akipeana mkono na Kiongozi wa Msafara wa baadhi ya Wabunge kutoka Uganda Mhe. Cecilia Barbara wakati wa ziara yao katika Taasisi hiyo kwa lengo la kujifunza leo Jijini Dar es Salaam.
KC2
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Profesa. Mohamed Janabi akielezea jambo wakati wa ziara ya Wajumbe wa Kamati ya Huduma za Jamii wa Bunge la Uganda waliotembelea Taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam. Wabunge hao wametembelea Taasisi hiyo ili kujionea namna inavyofanya majukumu yake.
KC3
Mwenyekiti wa Kudumu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mussa Zungu akizungumza jambo mbele ya Wabunge kutoka Uganda walipotembelea Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) leo Jijini Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni Kiongozi wa Msafara wa Wabunge kutoka Uganda Mhe. Cecilia Barbara na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Profesa. Mohamed Janabi (katikati).
KC4
Baadhi ya Wabunge kutoka Uganda wakifuatilia Maelezo kuhusu namna Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) inavyofanya kazi wakati wa ziara yao katika Taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam.
KC5
Baadhi ya Wabunge kutoka Uganda wakiwa katika sehemu ya mapokezi ya kuingia Wodi ya Watoto katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) leo Jijini Dar es Salaam.
KC6
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Profesa. Mohamed Janabi (mwenye tai nyekundu) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wabunge kutoka Uganda walipotembelea Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) kwa lengo la kujifunza leo Jijini Dar es Salaam.Picha zote: Frank Shija – MAELEZO

No comments :

Post a Comment