Naibu Kamishna wa forodha na
Maboresho ya Vihatarishi Hatari wa Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA, Bw.
James Mbunda (Kushoto) na akizungumza na Mwakilishi Mkazi wa Ubalozi wa
China anayeshughulikia Uchumi na Biashara, Bw. Lin Zhiyong, wakati wa
kufungua mafunzo kuhusu Takwimu na kudhibiti Vihatarishi hatari vya
Forodha, yanayotolewa na Chuo cha Forodha cha Shanghai-China, Jijini Dar
es Salaam.
Mkurugenzi Msaidizi wa Rasilimali
watu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Grace Sheshui akiwakaribisha
watoa mafunzo ya Takwimu na Udhibiti Vihatarishi hatari vya Forodha,
yanayotolewa na Chuo cha Forodha cha Shanghai-China, Jijini Dar es
Salaam.
Naibu Kamishna wa Forodha na
Maboresho ya Vihatarishi Hatari wa Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA, Bw.
James Mbunda, akizungumza na watoa mafunzo ya Takwimu na Udhibiti
Vihatarishi hatari vya Forodha, yanayotolewa na Chuo cha Forodha cha
Shanghai-China, Jijini Dar es Salaam, kushoto kwake ni Mwakilishi Mkazi
wa Ubalozi wa China anayeshughulikia Uchumi na Biashara, Bw. Lin
Zhiyong.
Baadhi ya maafisa kutoka Wizara
ya Fedha na Mipango wakisikiliza kwa makini maelezo ya awali ya mafunzo
ya kutoka kwa Mwakilishi Mkazi wa Ubalozi wa China anayeshughulikia
Uchumi na Biashara, Bw. Lin Zhiyong, katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na
Mipango, Jijini Dar es Salaam.
Maafisa kutoka Wizara ya Fedha na
Mipango na wengine (kulia) na wakufunzi wa Takwimu na Udhibiti
Vihatarishi hatari vya Forodha wakisikiliza maelezo ya awali wakati wa
ufunguzi wa mafunzo hayo katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango
Jijini Dar es Salaam.
Mkufunzi Mkuu wa masuala ya
forodha kutoka Chuo cha Forodha cha Shanghai, China, Profesa Sun Hao
(kulia) akizungumza jambo wakati wa hafla ya ufunguzi wa mafunzo ya siku
14 ya maafisa wa Forodha kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA, katika
ukumbi wa mikutano wa Wizara ya Fedha na Mipango, Jijini Dae Salaam.
Naibu Kamishna wa Forodha na
Maboresho ya Vihatarishi Hatari wa Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA, Bw.
James Mbunda (wa tatu kulia) akiwa katika picha ya pamoja na wakufunzi,
pamoja na maafisa wa forodha kutoka TRA, baada ya ufunguzi wa mafunzo ya
siku 14 kuhusu masuala ya forodha, katika ukumbi wa Wizara ya fedha na
Mipango, Jijini, Dar es Salaam.
Mwakilishi Mkazi wa Ubalozi wa
China anayeshughulikia Uchumi na Biashara, Bw. Lin Zhiyong (Kushoto) na
Mkurugenzi Msaidizi wa Rasilimali watu wa Wizara ya Fedha na Mipango,
Bi. Grace Sheshui (kulia) wakipeana mkono baada ya ufunguzi wa mafunzo
ya masuala ya forodha yanayotolewa na Chuo cha Forodha cha Shanghai,
China, mafunzo yanayofanyika katika Ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango
Jijini Dar es Salaam.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-WFM)
No comments :
Post a Comment